• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MHE. MTANDA AWATAKA ASKARI WALIOFANYA VIZURI 2024 KUWA CHACHU KWA WENGINE 2025

Posted on: February 8th, 2025

MHE. MTANDA AWATAKA ASKARI WALIOFANYA VIZURI 2024 KUWA CHACHU KWA WENGINE 2025


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewapongeza Wakaguzi na Askari wote wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza waliotekeleza vizuri zaidi kwenye majukumu yao katika maeneo yao ya kazi hivyo kupelekea kupata vyeti vya Sifa na zawadi kwa mwaka 2024.

Mhe. Mtanda ametoa pongezi hizo leo Februari 08, 2025 alipokuwa akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Familia ya Polisi 2025 yaliyoadhimishwa katika viwanja vya FFU Mabatini, Jijini Mwanza na kuwataka Maafisa na Askari waliofanya vizuri kuwa chachu kwa wengine ambao hawakufanya vizuri.

Aidha RC Mtanda amewapongeza na kuwasihi kuendelea na ari na moyo huo wa kuchapa kazi kwa bidii, uaminifu, nidhamu na maarifa ya kupigiwa mfano, ujasiri, kujituma, kupenda kazi, kuwa na kauli nzuri na kutoa huduma nzuri inayozingatia haki kwa wananchi.

Kadhalika Mhe. Mtanda amesema Vyeti vya Sifa na zawadi zilizotolewa leo siku ya Familia ya Polisi ni kumbukumbu kwa sisi tuliopo na wanaokuja kwamba hawa Wakaguzi na Askari ni miongoni mwa Askari waliolifanyia vizuri zaidi katika jeshi la polisi na Wananchi kwa ujumla kwa mwaka 2024/2025.

“Ni matumaini yangu kuwa mafanikio yao yatakuwa kichocheo kwa Askari wengine ambao hawakupata vyeti vya Sifa na zawadi leo kuongeza bidii zaidi ili waweze kufikia na hata kuzidi viwango vya ubora wa kufanya kazi vizuri zaidi”.

Mhe. Mtanda pia amesema tunajivunia mchango mkubwa unaotolewa na Jeshi la Polisi katika kulinda usalama pamoja na maisha na mali za raia. Amesema anatambua kazi kubwa na nzuri waifanyayo iliyotufikisha hapa tulipo sasa.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza DCP Wilbrodi Mtafungwa amesema maadhimisho ya Siku ya Familia ya Polisi ni kiashiria cha kuwa mwaka mpya wa Kipolisi umefunguliwa rasmi amabapo wanashiriki pamoja kama familia kuadhimisha sherehe hiyo.

DCP Mtafungwa ameendelea kwa kusema kuwa zawadi zilizotolewa ni namna ya kutambua mchango na kazi nzuri iliyofanywa na Askari pamoja na Maafisa hao katika kutekeleza majuku ya jeshi la polisi la kulinda usalama wa raia na mali zao.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti