• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Mhe Ngaga ampongeza Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza kwa msaada wa Madawati 105 Halmashauri ya Buchosa

Posted on: October 23rd, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga amemshukuru Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana na marafiki zake kwa msaada wa Madawati 105 kwa shule za Msingi Nyehunge na Mtakuja zilizopo Wilayani humo.

Akizungumza mbele ya kamati za Shule hizo zilizopo Halmashauri ya Buchosa,Mkuu huyo wa Wilaya amesema huo ni mfano wa kuigwa kwa watu wengine kuona umuhimu wa kujitoa pale unapokuwa na nafasi kuchangia Maendeleo ya Taifa letu.

"Balandya amesoma shule hii ya Nyehunge kwa kutambua umuhimu wa elimu ameona ni vyema atoe mchango huu wa Madawati haya ambayo yatachangia watoto wetu kusoma katika mazingira bora na hatimaye kuwepo na ufaulu mzuri wa masomo" amesema Mhe Ngaga.

Awali akizungumza kwa niaba ya Bw. Balandya Elikana, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Rasilimaliwatu Bw. Daniel Machunda amebainisha msaada wa Madawati hayo ni kuuunga mkono kwa vitendo Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan ambayo imejikita kuendeleza elimu nchini kwa kila mtoto aweze kupata nafasi ya kusoma.

 Bw. Machunda amesema awamu ya kwanza February mwaka huu Balandya akishirikiana na wafanyakazi wenzake aliofanya nao kazi Idara ya Menejimenti ya Bajeti kutoka Wizara ya Fedha na Mipango walifanikisha utengenezaji wa Madawati 120 yaliyogawiwa shule za Msingi Nyehunge,Bukiliguli na Ng'wabasabi,Madawati ambayo yamewanufaisha wanafunzi kati ya 210 hadi 315.

"Tumeona dhamira ya dhati ya Rais wetu katika kuleta maendeleo kwa kuondoa michango shuleni na wanafunzi kusoma bure kuanzia kidato cha kwanza hadi cha Sita na kuziboresha shule zote za Serikali,tunapoonesha kuunga mkono jitihada zake tunazidi kumpa ari ya kuwapigania wananchi wake kusonga mbele katika nyanja zote ikiwemo kielimu na kiuchumi" amesisitiza Machunda.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Buchosa Julius Mlongo amesema kata ya Nyehunge ina jumla ya shule 10 za Msingi kati ya hizo 8 zinamilikiwa na Serikali na 2 ni za binafsi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw Balandya Elikana amesoma shule ya Msingi Nyehunge kuanzia mwaka 1978 na kihitimu elimu ya msingi mwaka 1984.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti