• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania Bara,Rai ya ujenzi wa Taifa imara yatolewa Mwanza

Posted on: December 9th, 2022

*Maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania Bara,Rai ya ujenzi wa Taifa imara yatolewa Mwanza.


Maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania Bara yamefanyika leo nchini huku Rai ya kuthamini amani na umoja na kulijenga Taifa kiuchumi ikihimizwa kwa Watanzania.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndg.Balandya Elikana akizungumza katika maadhimisho hayo Wilayani Magu amesema  hakutakuwa na maana kama tunafanya maadhimisho haya huku amani miongoni mwa Watanzania ikiwa hakuna ni dhahiri Taifa haliwezi kuwa na Maendeleo yoyote.

Amesema Nchi yetu imebarikiwa kuwa na amani na umoja ulioasisiwa na Viongozi wetu Baba wa Taifa Hayati Julius Nyerere na Abeid Karume na tumeendelea kuona maendeleo ndani ya Taifa letu tangu Uhuru hadi sasa.

"Wakati wa miaka ya Uhuru Mkoa wa Mwanza ulikuwa na shule za Sekondari 5 lakini sasa tunazo 317,Hospitali zilikuwa 3 za Wilaya lakini sasa tunazo 26 wakati huduma ya maji ilikuwa inawafikia watu kwa asilimia 19 lakini sasa ni asilimia 60 Wananchi wanapata rasilimali hiyo" amesema Mtendaji huyo Mkuu wa Mkoa.

Amewakumbusha wananchi kuendelea kuwaenzi kwa vitendo Viongozi wetu waliopigania Maendeleo ya Taifa hili kwa kufanya kazi kwa bidii,ubunifu na kutanguliza uzalendo.

"Tunaona kasi ya maendeleo inayofanywa na Rais wetu Dkt.Samia Suluhu Hassan,kila mwananchi ana kila sababu ya kuunga mkono jitihada hizi ambazo ni kwa faida yetu na vizazi vijavyo"amesisitiza Ndg.Balandya

Awali akitoa salamu za Wilaya ya Magu Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Salum Kalli amesema Miradi mingi katika nyanja mbalimbali ikiwemo ya afya na shule imetokana na uimara wa Serikali ya awamu ya Sita ambayo imeonesha kwa vitendo dhamira ya kumletea maendeleo mwananchi.

Maadhimisho hayo yaliyokwenda pamoja na Mdhahalo uliolenga tumetoka wapi,tulipo sasa na tunakwenda wapi tangu kupata Uhuru wa Tanzania Bara,"Tujifunze kutanguliza uzalendo,kuepuka tamaa na kuridhika na kipato halali,kwa kufanya hivyo tutaepuka rushwa na kujenga Taifa lenye weledi"Mchungaji Dkt.Jacob Mutash.

"Tujenge utamaduni wa kuwapenda Viongozi wetu,tuwakosoe kwa busara na kuepukana na siasa za kusigana na chuki tukizingatia haya tutazidi kuwaenzi kwa vitendo waasisi wetu ambao miongozo yao imezidi kutuimarisha siku hadi siku"Padri John Kasembo mwalimu na mshauri wa viongozi.

Tanzania Bara imepata Uhuru wake Disemba 9 1961 kutoka kwa mkoloni Muingereza,huku kila mwaka yakifanyika maadhimisho hayo kwa kushiriki shughuli mbalimbali za ujenzi wa Taifa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti