• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MIKOPO KWA WAFANYA BIASHARA WADOGO MWANZA IHARAKISHWE- WAZIRI GWAJIMA

Posted on: February 10th, 2025

MIKOPO KWA WAFANYA BIASHARA WADOGO MWANZA IHARAKISHWE- WAZIRI GWAJIMA


Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima ametaka zoezi la utoaji wa mikopo kwa wafanyabiashara wadogo mkoani Mwanza lifanyike haraka kwani tayari Serikali imetoa fedha Tshs. bilioni 5.

Akizungumza leo Februari 10, 2025 kwenye ukumbi wa Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza na viongozi wa Shirikisho la wafanyabiashara hao SHIUMA katika mkutano wa dharura, Waziri Gwajima ametoa maelekezo kuanzia ngazi ya Wizara yake,Mkoa na Halmashauri kuhakikisha mchakato wa awali wa usajili na hatimaye kupata vitambulisho ili wapate mikopo hiyo ukamilike haraka.

Awali kiongozi huyo mwandamizi wa Serikali mara baada ya kusomewa taarifa za usajili za wafanyabiashara hao kwenye Halmashauri zote za Mkoa wa Mwanza alionesha kutoridhishwa na idadi ndogo huku kasi ya usajili ikienda kwa kusua sua.

"Hii hali siwezi kuikubali licha ya kikao hiki cha dharura,nimewasikia watenda wote nilichokibaini ni baadhi kushindwa kutekeleza majukumu yao na mwishowe ni kuwachonganisha wafanyabiashara hao na Mhe.Rais,hii siyo sawa," Waziri Gwajima.

Kuhusu Mwanza kutopata Ofisi ya Shirikisho la SHIUMA, licha ya fedha kuletwa mkoani humo mara baada ya Rais kuridhia kutoa fedha kwa mikoa yote ya Tanzania Bara, amewataka viongozi hao kuandika barua kwa kufuata taratibu zote na nakala apatiwe ili aweze kupata nafasi ya kuijengea hoja suala lao na siyo kufanya mawasiliano kwa njia ya simu pekee.

Afisa Maendeleo ya Jamii mkoani Mwanza Bi.Janeth Shishila ameomba Wizara ione namna ya kuwawezesha vifaa zikiwemo Kompyuta maafisa maendeleo ngazi ya kata ambapo mchakato huo wa usajili unaanzia huko.

"Hali ya kusua sua usajili wa wafanyabiashara wadogo imechangiwa na watendaji kukosa vitendea kazi vya msingi na hakuna kifungu kinachowapa fedha huko kwenye halmashauri," amesisitiza Bi.Janeth.

"Tunamshukuru Rais kwa nia yake njema kwetu sisi wafanyabiashara wadogo lakini wapo baadhi wanao fanya hujuma ili hizi fedha zishindwe kuwafikia walengwa na kunufaika wasiohusika." Msemaji wa Shirikisho la wafanyabiashara, Jumanne Ayoub.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti