• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MIRADI YA ZAIDI YA SHS BILIONI 2 YAKAGULIWA H/YA BUCHOSA,RAS MWANZA ATOA MAAGIZO

Posted on: September 13th, 2024

MIRADI YA ZAIDI YA SHS BILIONI 2 YAKAGULIWA H/YA BUCHOSA,RAS MWANZA ATOA MAAGIZO


Halmashauri ya Buchosa Wilayani Sengerema imepewa maagizo ya kuharakisha miradi ya maendeleo na pia kusimamia na kufuatilia miradi ya vijana inayotokana na mikopo ya asilimia.

Rai hiyo imetolewa leo Septemba 13,2024 na Katibu Tawala wa mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana alipofanya ukaguzi wa baadhi ya miradi yenye thamani ya zaidi ya shs bilioni mbili na kusisitiza ni lazima ikamilike kwa wakati ili iwe na tija kwa wananchi.

Akiwa kwenye kituo cha afya Nyakasungwa kilichogharimu shs milioni 250 fedha zilizotokana na mapato ya ndani lakini bado hakijaingiziwa umeme na maji,mtendaji huyo wa Mkoa amemtaka mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Benson Mihayo kukaa na Taasisi husika ili kukamilisha haraka.

"Hiki kituo ni lazima kiwe na maji muda wote na pia akiba ya maji kutokana na aina ya kazi yake,fanyeni utaratibu wa kuvuna maji ya mvua ili kujiwekea akiba,"Balandya.

Amesema Serikali ya awamu ya sita inazidi kuiboresha sekta ya afya hivyo anaamini kwa juhudi za halmashauri hiyo kituo hicho kitakuja kutoa huduma bora kwa wananchi

Kuhusu miradi ya vijana inayotokana na mkopo wa asilimia kumi amevipongeza vikundi vinavyofanya vizuri na kurejesha fedha kwa wakati lakini akawakumbusha Maafisa mipango kuweka utaratibu wa kuwasimamia vyema ili fedha hizo za mkopo ziwanufaishe na wengine.

Aidha amemtaka Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Senyi Ngaga kuwaelimisha wananchi kutumia maji safi na salama waliyowekewa na Serikali baada ya kupata taarifa ya baadhi ya wananchi kutoyapenda maji hayo na kuyatumia yale yasiyo salama kwa madai yaliyowekewa dawa ya kuuwa vijidudu hayana ladha.

Katibu Tawala huyo anaendelea na zoezi la kukagua miradi ya maendeleo na Septemba 14,2024 atakuwa Halmashauri ya Sengerema.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti