• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Miti zaidi ya 10,000,000 yapandwa Mkoani Mwanza

Posted on: February 23rd, 2023


Mkoa wa Mwanza umefanikiwa kupanda miti zaidi ya 10,000,000 ikiwa ni utekelezaji wa mkakati wa kutunza mazingira na kuhifadhi vyanzo vya maji na kutekeleza agizo la Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango aliyoitaka mikoa yote nchini kupanda miti ili kutunza mazingira.

Hayo yameelezwa leo Februari 22, 2023 jijini hapa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima wakati akitoa taarifa ya utunzaji mazingira mbele ya Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhe. Khamis Hamza Khamis ambaye yuko katika ziara ya kikazi mkoani hapa.

Mhe. Malima amesema wameshirikiana na Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) katika kufanikisha hilo huku mikakati ikiwa ni kupanda miti zaidi ya 50,000,000 ndani ya miaka mitano, ambapo miti hiyo imepandwa kwenye Taasisi ikiwamo shule.

“Tumewapa TFS (Wakala wa Misitu Tanzania) tenda ya kupanda miti hiyo na tumeanza kwenye shule tunaamini tutafanikiwa kwa sababu TFS wana utaalam wa kujua miti gani inayoweza kustawi katika maeneo yapi.

Kikubwa katika upandaji wa miti ni Changamoto inayotukabili ni uhaba wa maji ya kuimwagilia kwani miti mingi imepandwa maeneo ya vijijini,” amesema Mhe. Malima.

Akizungumzia kuhusu uchafuzi wa mazingira hususani nyumba za ibada na maeneo ya starehe katikati ya makazi ya watu, Mhe. Malima ameliagiza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kufanya ukaguzi kwenye maeneo hayo ili kujiridhisha kama vigezo vinazingatiwa.

“Piteni kwenye hayo maeneo yote mpite na  ‘sound meter’ hatuwezi kupigiwa kelele hadi saa 7 usiku wakati kuna watoto na wagonjwa wanaohitaji kupumzika muda huo, Mwanza ni jiji kubwa tukitaka kulifanya livutie lazima tujiwekee taratibu,” ameagiza.

Kwa upande wake, Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Khamis Hamza Khamis amevitaka viwanda vyote nchini kutekeleza sera ya mazingira kwa kutumia teknolojia ya kisasa ili kutunza mazingira huku akivitaka kutenga fungu maalumu kusaidia shughuli zote za mazingira katika maeneo husika ikiwemo usafi, upandaji miti na kutoa elimu inayohusu mazingira.

“Tuachane na kutumia makaa ya miti tutumie teknolojia ya kisasa itakayotusaidia kulinda mazingira, wenye viwanda wahakikishe hawatiririshi maji machafu au yenye sumu kwenda kwenye makazi ya watu na kuleta athari kwa wananchi. Pia mhakikishe moshi hauleti kero kwa wananchi, tukigundua unafanya hivyo na kuwasabaishia athari za kiafya tutachukuliana hatua za kisheria,” amesema Naibu Waziri.

Katika ziara yake ya kikazi jijini Mwanza Naibu Waziri Khamis Hamza Khamis ametembelea mradi wa dampo la kisasa uliopo Kata ya Buhongwa na kiwanda cha Multi Cable LTD. kilichopo Kata ya Mhandu Wilaya ya Nyamagana kinachozalisha bidhaa za plastiki.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti