• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Mkuu wa Mkoa Mwanza ahimiza huduma za maji kwenye Vituo vya kutolea huduma za afya/elimu

Posted on: March 2nd, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima ameziagiza Halmashauri na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) kushirikiana kupeleka Maji safi na salama kwenye vituo vyote vya kutolea huduma za afya pamoja na taasisi za Elimu mkoani humo ili kupunguza adha kwa watumishi na wananchi wanaopata huduma.

Akikaguzi Maendeleo ya Ujenzi wa Kituo cha Afya Buzilasoga wilayani Sengerema unaotarajia kuwahudumia zaidi ya wananchi 1852 chini ya Mpango wa kunusuru Kaya Masikini (TASAF III) kwa zaidi ya Milioni 543, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amesema huduma za Afya haziwezi kutolewa pasipo kuwa na Maji ya kutosha.

Amesema pamoja na fedha za Mradi huo kuhusisha Ujenzi wa Miundombinu kama vile Wodi ya Wazazi, Watoto, Maabara na Jengo la Kupokelea wagonjwa wa nje ni lazima Halmashauri na RUWASA kushirikiana kutafuta fedha za kuchimba kisima kirefu cha maji mara moja kabla ya kuanza kwa kutoa huduma.

"Kituo cha Afya bila huduma za Maji haiwezekani na tusidanganyane na kutegemea chanzo cha maji ya mvua badala yake naomba Halmashauri itenge angalau Milioni 30 hapa ili tupate kisima  kirefu cha maji kwenye kituo hiki." Amesema Malima.

Aidha, ameagiza Halmashauri hiyo kuongeza muda wa kufanya kazi na Rasilimaliwatu ili hadi kufikia Machi 15, 2023 mradi huo uwe umekamilika na ili kuweza kutimiza vigezo vya kuendelea kupata ufadhili wa miradi mingine ya maendeleo.

Naye, Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana amewataka wananchi wa kijiji cha Mami kilichopo kata ya Kishinda kuendelea kujitolea nguvu kazi kwenye mradi ya Maji wa Zahanati ya Kijiji ambapo Mkuu wa Mkoa amechangia Shilingi Laki 5 kuunga mkono juhudi za wanamchi wanaochimba mtaro wa Maji.

"Mhe. Mkuu wa Mkuu, Mradi huu umefikia Asilimia 80 ya Ujenzi na tunatarajia kuukamilisha baada ya wiki moja" Amesema Ndugu. Malisa Nguda, Mratibu wa TASAF Wilaya ya Sengerema.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti