• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MKUU WA MKOA MWANZA AWASHUKURU KANISA LA AICT UWEKEZAJI SEKTA YA AFYA

Posted on: February 8th, 2025

MKUU WA MKOA MWANZA AWASHUKURU KANISA LA AICT UWEKEZAJI SEKTA YA AFYA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amelipongeza Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT) kwa usimamizi na uendeshaji wa meli ya matibabu kwa kutoa huduma za afya

katika visiwa vya ziwa victoria kwa zaidi ya miaka 10.

Mhe. Mtanda ametoa pongezi hizo leo Februari 08, 2025 wakati wa Maadhimisho ya miaka kumi ya mpango wa meli ya matibabu ya MV Jubilee Hope Medical Ship na uzinduzi wa meli ya matibabu ya MV. Lady Jean yaliyofanyika katika viwanja vya Rock Beach Jijini Mwanza.

Mkuu wa Mkoa amewashukuru pia Washirika katika uendeshaji wa meli ya matibabu Vinetrust, (Geita Gold Mining Ltd – GGML), hivyo kufanikisha safari ya miaka 10 katika kutoa huduma za afya

katika visiwa vya ziwa victoria.

Sambamba na hilo ametoa shukrani za dhati kwa wadau wengine ambao ni Vine Trust UK kwa kushikiriana na Babcok kwa kufanikisha upatikanaji wa meli nyingine ya matibabu ambayo itasaidia kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma za afya kwenye Visiwa vya Ziwa Viktoria.

“Kwa kipindi cha miaka kumi, MV. Jubilee Hope imekuwa msaada mkubwa kwa jamii, ikitoa huduma za afya kwa maelfu ya watanzania waliopo visiwani ndani ya Ziwa Viktoria, ambako huduma za afya zilikuwa na changamoto katika upatikanaji wake”.

Kupitia huduma hizi, tumeshuhudia mafanikio makubwa katika kupunguza magonjwa, kuokoa maisha, na kuboresha ustawi wa jamii kwa ujumla. Ameongeza Mhe. Mtanda.

Kadhalika Mkuu wa Mkoa amesema Uzinduzi wa MV. Lady Jean ni Hatua Mpya ya Maendeleo katika kuendeleza huduma za matibabu kwa wakazi wa Ziwa Viktoria.

Ambapo Meli hiyo mpya itaimarisha juhudi za huduma za afya kwa jamii ya visiwani kwa Kupanua wigo wa utoaji wa huduma za matibabu kwa idadi kubwa zaidi ya wagonjwa 7, Kuboresha utoaji wa huduma za dharura kwa haraka na kwa ufanisi mkubwa zaidi.

“Hivyo, tunawashukuru sana kanisa la AICT kwa kuja na mradi wa Afya kupitia meli hii ya Matibabu ya MV. Lady Jean”.

Naye Askofu wa Kanisa la AICT Mussa Magwesela, amesema anaishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ushirikiano wanaoupata kuanzia walipoanza rasmi shughuli za utoaji wa matibabu kwa njia ya Meli ambapo kwa takribani miaka 10 sasa tangu pale walipoanza rasmi mnamo mwaka 2015

Kadhalika amesema Kwa miaka kumi iliyopita, wanajivunia mafanikio kama vile Huduma za afya zimetolewa kwa zaidi ya watu 500,000 katika visiwa vya ziwa Viktoria kwenye utoaji wa chanjo, matibabu ya malaria, huduma za afya ya uzazi, upasuaji mdogo na huduma za afya ya kinywa na meno.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti