• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MWANZA NI SEHEMU SAHIHI YA UWEKEZAJI - RC MTANDA

Posted on: April 10th, 2025

MWANZA NI SEHEMU SAHIHI YA UWEKEZAJI - RC MTANDA


Serikali ya Mkoa wa Mwanza imewakaribisha na kuwahakikishia ushirikiano wa dhati Wawekezaji na Wafanyabiashara wote wanaotamani kuja kufanya biashara na uwekezaji katika Mkoa wa Mwanza ikiwa ni kwa mustakabali wa kukuza biashara na uchumi wa Mkoa na Taifa kwa ujumla.

Kauli hiyo imetolewa leo Aprili 10, 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda alipokuwa akifungua Semina ya uhamasishaji wa masuala ya ushindani yenye lengo la kumlinda mlaji wa bidhaa bandia kwa wazalishaji wa Jiji la Mwanza, ambapo amewashukuru Tume ya ushindani (FCC) kwa kufungua Ofisi ya Kanda Mkoani Mwanza.

Mkuu wa Mkoa amesema kwa kufungua Ofisi katika Mkoa wa Mwanza inaongeza juhudi, kuleta huduma karibu na wananchi na kufanya utekelezaji wa majukumu kwa mujibu wa sheria hususani katika masuala ya ushindani, udhibiti wa bidhaa bandia na kumlinda mlaji kwa ujumla.

“Kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi iliyofanyika tarehe 23 Agosti, 2022 Mkoa wa Mwanza una jumla ya watu 3,699,872 Idadi hii ya watu ni fursa katika masoko na biashara ukizingatia pia Mkoa wa Mwanza ni wa pili kwa idadi ya watu ukitanguliwa na Mkoa wa Dar es Salaam”.

Aidha Mkuu wa Mkoa amesema kiuchumi Mkoa wa Mwanza unachangia kwenye pato la Taifa (GDP) kwa Trilioni 13.59. ukiwa ni Mkoa wa Pili kwa kuchangia kwa asilimia kubwa kwenye pato la Taifa, ambapo Mkoa wa Mwanza unachangia kwa asilimia 7.2.

Sambamba na hayo Mhe. Mtanda ameeleza kuwa uchumi wa Mkoa wa Mwanza unachangiwa na Kilimo 75% (mazao, mifugo na misitu); huduma 10% (biashara, hoteli, usafirishaji, mawasiliano, taasisi za kifedha, kodi za pango, elimu, afya, na utawala); Uvuvi 7% na viwanda na ujenzi 8% (madini, umeme, maji, ujenzi na uzalishali).

“Nimeelezea uchumi wa Mkoa kwa uchache na takwimu si kwa sababu mimi ni bingwa wa Takwimu, hapana, bali nimefanya hivyo ili muweze kupata picha halisi ya uchumi wa Mkoa lengo likiwa mkiwa kama sekta ya biashara kwa pamoja muone namna bora ya kuzitumia vizuri fursa za kiuchumi zilizopo”.

Kadhalika Mkuu wa Mkoa amewaomba FCC haswa walio katika Kanda ya Mwanza kushirikiana pamoja na kwa ukaribu ili kuhakikisha masuala ya kiushindani yanasikilizwa na yanatatuliwa kwa wakati na wananchi wanapewa elimu zaidi kuhusu masuala ya ushindani, kumlinda mlaji na mapambano dhidi ya bidhaa bandia.

kabla ya kufungua semina hiyo Mkuu wa Mkoa amewataka wafanyabiashara waliopata fursa ya kuhudhuria semina hiyo kwenda kuitumia vizuri elimu watakayopata na kuwa mabalozi wazuri wa FCC katika kuwaelimisha wafanyabiashara, wazalishaji wenye viwanda wengine na wananchi kwa ujumla ambao hawakupata fursa ya kuhudhuria mafunzo hayo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti