• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Mwanza wafaidika na vifaa vya uokoaji wakati wa majanga

Posted on: November 27th, 2018

Taasisi ya SUKOS KOVA Tanzania na Vodacom Tanzania wametoa vifaa vya uokoaji kama vile Vifaa vya kuzimia moto,Vifaa vya kuogelea vyenye thamani ya Shilingi  Milioni 120 wilayani Nyamagana,wanufaika wakiwa Jeshi la Zima moto, Wavuvi Shule ya Msingi Nyamagana, Sweya na Luchelele

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo Mkuuu wa wilaya ya Nyamagana Dkt Phillis Nyimbi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella amewashukuru wadhamini wa vifaa hivyo kwa nia yao njema ya kusaidia watu wa kanda ya ziwa kuweza kujiokoa na majanga mbali mbali yanayoweza kujitokeza 

"Nimshukuru Mkurugenzi wa SUKOS KOVA na Vodacom Tanzania kwa nia yao njema ya kuwasaidia wana Mwanza.Hivi vifaa vikitumiwa ilivyokusudiwa itasaidia kupunguza na kutuepusha na baadhi ya majanga" amesema Dr Nyimbi

Aidha Dr Nyimbi amewataka watu wote waliopata vifaa hivyo vikatunzwe vyema na kutumika kwa maslai ya wengi na sio watu binafsi .

Akiongea kwa niaba ya Taasisi ya SUKOS KOVA foundation, Kamishna mstaafu wa Jeshi la Polisi Suleman Kova amesema ameguswa na kuona ni vyema Taasisi yake kujikita kutoa Elimu na vifaa kwa watanzania namna ya kujikinga na kujiokoa na majanga mbali mbali yanayotokea kwenye jamii zetu.

Hata hivyo Ndg Kova amewataka wadau wengine kuiga mfano wa Vodacom Tanzania na kuchangia vifaa mbali mbali kwa ajili ya kusaidia uokoaji wakati wa majanga,

Akitoa salam za Halmashauri ya Jiji la Mwanza Naibu Meya wa Jiji la Mwanza Mhe Bhiku kotecha amewashukuru wadau hao wa maendeleo kwa kulichagua Jiji la Mwanza na hususan Kata ya Nyamagana kuwa sehemu ya uzinduzi wa programu hiyo.

Pamoja na hilo, Mhe Kotecha amesema ataendelea kuwa balozi mzuri wa Vodacom Tanzania kutokana na Vodacom kutoa mchango mkubwa mara kwa mara kusaidia jamii.

Naibu meya ameendelea kuwaomba Vodacom Tanzania kuja kuwekeza kwenye uwanja wa kisasa wa mpira wa miguu wilayani Nyamagana kwa kujenga majukwaa ya kukaa watu nao pia watapata fursa ya kutangaza matangazo yao ya biashara.



Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti