• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MWANZA WAONGOZA MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU KANDA YA ZIWA

Posted on: August 20th, 2024

MWANZA WAONGOZA MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU KANDA YA ZIWA


Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Emily Kasagara leo Agosti 20, 2024 ametangaza matokeo ya utamilifu kidato cha nne kwa mikoa ya kanda ya ziwa ya Geita, Simiyu, Kagera, Mara na Mwanza yenye ufaulu wa GPA 3.9 kwa asilimia 84.48 (Daraja la kwanza hadi la nne).

Akitangaza matokeo hayo Kasagara amefafanua kuwa ufaulu wenye tija daraja I- III ni asilimia 26.48 GPA ya 2.4 na kwamba ufaulu umejikita katika daraja la 4 kwa asilimia 13.01 huku daraja sifuri ni asilimia 9.02 na akawataka walimu kuwajibika ili kupandisha ufaulu hususani madaraja 1, 2 na 3.

"Mkoa wa Mwanza umeongoza kwa GPA ya 3.72 kwa asilimia ya ufaulu wa asilimia 86.13 ikifuatiwa na Mkoa wa Simiyu na tunazipongeza halmashauri za Manispaa ya Ilemela, Jili la Mwanza na Bukombe DC kwa kufanya vizuri." Amesema Kasagara.

Vilevile, ndugu Kasagara ameipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa kuamini kuwa elimu ndio nyenzo ya kuaminika inayowezesha kila mtu kuyakabili mazingira yake kwa usahihi kwa kujipatia maendeleo endelevu kwa kutoa fedha za elimu bila ada kwa shule za msingi na sekondari jambo linalochangia kukuza ufaulu.

"Serikali imeendelea kuimarisha miundombinu kwa kukarabati shule kongwe na kujenga shule mpya na kuongeza miundombinu kama madarasa, mabweni, maabara na vyoo." Ameongeza Kasagara.

Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza Martin Nkwabi amefafanua kuwa malengo ya mitihani hiyo siyo kujikita tu kwenye kuona mwanafunzi amefeli au amefaulu bali ni kujipima kwenye ufundishaji wa walimu ili kurekebisha kasoro kwa ajili ya kufanya vizuri kwenye mitihani wa mwisho ya kumaliza elimu ya sekondari.

Aidha, amewataka walimu kuwajibika kuhakikisha wanapandisha matokeo kwa watoto kwenye madaraja ya kwanza hadi la tatu kama walivyowekeana malengo hususani mkoa wa Mwanza ili kuhakikisha wanafuta daraja ziro na kupunguza daraja la nne kwa wanafunzi.

"Nataka kila mkuu wa shule afanye tathmini na akatafute sababu ya matokeo aliyoyapata na kuhakikisha anarekebisha kasoro hizo ili tupate ufaulu wa zaidi ya asilimia 60 kwa wanafunzi wetu ili kuhakikisha tunafuta daraja ziro na daraja la nne." Afisa Elimu Mkoa.

Matokeo hayo ya mtihani uliofanyika  Julai mwaka huu yanapatikana kupitia https://sras.ac.tz ambapo kila mmoja anaweza kuona na yamepangwa kwa mpangilio wa mikoa, halmashauri na shule.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti