• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MWANZA WATOA MAONI YA NAMNA BORA YA KUKUSANYA KODI NCHINI

Posted on: January 13th, 2025

MWANZA WATOA MAONI YA NAMNA BORA YA KUKUSANYA KODI NCHINI


Mwenyekiti wa Tume ya Rais ya Kukusanya maoni ya maborehso ya kodi Mhe. Balozi Ombeni Sefue ametoa rai kwa wafanyabiashara Mwanza kujenga tabia ya kulipa kodi ili kuipa nguvu Serikali na kuhakikisha inaweza kujitegemea kwa kuboresha miundombinu mathalani ya afya.

Ametoa wito huo leo Jumatatu tarehe 13 Januari, 2025 katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakati akifungua kikao cha wadau cha kukusanya, kupendekeza na kuwasilisha changamoto za masuala ya kodi nchini kilicholenga kuboresha namna bora ya pamoja ya kufikia malengo.

"Tanzania tija yetu ya kukusanya mapato bado ni ndogo ni kati ya asilimia 12 hadi 13 tu na haipaswi kuwa kuwa hivyo maana angalau tufikie asilimia 16 maana wananchi wanataka shule zijengwe, miundombinu ya afya iwepo tena ya kisasa je tutafikaje huko kama hatutakua na fedha." Mwenyekiti.

Mwenyekiti wa Chemba ya wafanya biashara Mwanza (TCCIA) Gabriel Chacha ametoa wito kwa Serikali kuondoa mfumo wa kukokotoa kodi ambao sio rafiki kwani haufuti taarifa za nyuma za uhai wa biashara na waondoe utitiri wa kodi kwenye biashara badala yake zilipwe kwenye mwamvuli mmoja.

"Changamoto nyingine ni sheria, faini na tozo hapa wafanyabiashara wanaumizwa sana na zinapaswa kupitiwa upya na kuzirekebisha maana adhabu zimewekwa kwa kiwango kimoja ambacho kinawaumiza moja kwa moja wajasiriamali." Ameongeza Bwana Chacha.

Wajumbe wengine wa tume hiyo ni Mhe. Balozi Maimiuna Tarishi Makamu Mwenyekiti wa Tume, Mhe. Balozi Mwanaid Maajar, Prof. Mussa Assad, Prof Florens Luoga, CPA. David Tarimo, CPA. Leonard Mususa, CPA. Rished Bade pamoja na CPA Abubakari Abubakar.

Tume hiyo imeundwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya kupokea maoni ya wadau juu ya kuwa na mfumo bora wa kukusanya mapato nchini pasipo malalamiko.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti