• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MWANZA YAADHIMISHA MIAKA 60 YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Posted on: April 26th, 2024

MWANZA YAADHIMISHA MIAKA 60 YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA


Mkoa wa Mwanza leo umeadhimisha miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano

 wa Tanzania,huku yakielezwa mafanikio mbalimbali ndani ya Muungano huo ukiwemo mshikamano miongoni mwa Watanzania na ukuaji wa shughuli za kiuchumi.

Akizungumza na wananchi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwenye viwanja vya Furahisha,Katibu Tawala wa Mkoa huo,Ndg. Balandya Elikana amebainisha mshikamano wa Kitaifa tulionao umeondoa ubaguzi licha ya kuwepo na wingi wa makabila hapa nchini.

"Ndugu wananchi tuna kila sababu ya kuulinda na kuutetea Muungano wetu,mtu wa kutoka Bara anaweza kwenda Zanzibar na mtu wa kutoka visiwani humo ana uwezo wa kuja huku bila ya vikwazo vyovyote,hali hii ndiyo imelijenga Taifa imara la Tanzania.

Amesema waasisi wa Muungano huu Hayati Baba wa Taifa,Julius Nyerere na Abeid Aman Karume tuwaenzi kwa kuzidi kuimarisha Umoja wetu huku ukileta tija kwa kila upande.

"Miongoni mwa mafanikio ya Muungano wetu tunaona miradi mbalimbali ya kuwaletea maendeleo wananchi ikifanyika,hapa Mwanza tuna ujenzi wa Reli ya kisasa SGR,Daraja la JP Magufuli,Meli ya Mv Mwanza na upanuzi wa uwanja wa ndege,"Balandya.

Aidha ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Samia kwa kuzidi kuimarisha sekta za afya,  elimu na kilimo tukiadhimisha miaka 60 ya Muungano tukiona sekta hizo zikizidi kuwa na tija kwa kuleta mageuzi ya kimaendeleo kwa wananchi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Ilemela ambapo sherehe hizo Kimkoa zimefanyika wilayani humo,Katibu Tawala wa Wilaya hiyo,Wakili Mariam Msengi amebainisha wameadhimisha sherehe hizo kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kufanya usafi sehemu kadhaa, kupanda miti na kufanya mashindano ya burudani.

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar umefanyika Aprili 26,1964 chini ya waasisi Hayati Julius Nyerere na Abeid Karume.

Kauli mbiu ya Maadhimisho ya miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano inasema Tumeshikamana,Tumeimarika kwa Maendeleo ya Taifa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti