• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MWAUWASA washauriwa kuja na huduma sahihi na bora mradi wa maji Butimba

Posted on: November 9th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima ameishauri Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira kukaa chini na kufanya tathmini makini kuhusiana na idadi halisi ya wakazi wa Jiji hilo ili miradi yake ya maji iwanufaishe wananchi wote.

Akizungumza na uongozi wa Mamlaka hiyo mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi wa chanzo cha maji Butimba,Mhe Malima amesema mara baada ya hesabu ya Sensa mwaka huu imeonesha Mwanza ina idadi ya watu milioni 4 hivyo mahitaji ya rasilimali hiyo itazidi kuwa kubwa.

"Nimemsikia hapa Meneja akisema mara baada ya mradi huo kukamilika utaweza kusambaza maji lita milioni 48 kwa siku hiyo haitoshi na Wananchi hawatawaelewa kuwa na mradi mkubwa namna hii halafu huduma ikawa bado hawaipati,ni lazima muone haja ya kufanya hesabu nzuri ili mradi huu uweze kutoa huduma kwa usahihi"amesema Mhe.Malima

Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha bado wakazi wa Jiji la Mwanza hasa waishio maeneo ya kwenye miinuko wanataabika kupata huduma ya maji kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uchakavu wa mtambo na maji kupotea njiani kabla ya kumfikia mwananchi.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa ameutaka uongozi wa MWAUWASA kumletea taarifa ya kimaandishi kuhusiana

mradi huo kuchelewa kukabidhiwa tofauti na muda waliokubaliana ambao ni Disemba mwaka huu na sasa utakabidhiwa Juni mwakani.

"Alivyokuja Mhe.Makamu wa Rais Philip Mpango kuzindua mradi huu aliambiwa hadi Disemba utakuwa umekamilika,sasa leo mmnanipa taarifa tofauti yenye sababu zenu za msingi za vifaa kuchelewa kuletwa kutoka kwa msambazaji kutoka nje ya nchi".Amesema Mkuu huyo wa Mkoa

Mkurugenzi Mtendaji wa MWAUWASA,Mhandisi Leonard Msenyele amesema maagizo yote yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wameyapokea na kuyatekeleza ili malengo ya kuwapatia huduma bora wananchi yatimie.

Mradi wa chanzo cha maji Butimba upo chini ya mkandarasi SOGEA SATOM kutoka Ufaransa na umegharimu jumla ya Shilingi Bilioni 69.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti