• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MWENGE WA UHURU WAIPONGEZA BUCHOSA KWA UHIFADHI WA MAZINGIRA, WAPANDA MITI ZAIDI YA MILIONI MOJA KWA MWAKA

Posted on: July 16th, 2023

MWENGE WA UHURU WAIPONGEZA BUCHOSA KWA UHIFADHI WA MAZINGIRA, WAPANDA MITI ZAIDI YA MILIONI MOJA KWA MWAKA


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 Ndugu Abdalla Shaibu Kaim ameipongeza Halmashauri ya wilaya ya Buchosa kwa juhudi kubwa wanazofanya katika kutunza na kuhifadhi mazingira.

Ndugu Kaimu ametoa pongezi hizo mapema leo katika shule ya Sekondari Bukokwa wakati akishiriki zoezi la upandaji miti 500 iliyotolewa na wakala wa huduma za misitu nchini (TFS) kati ya 1000 iliyopandwa kwenye shule hiyo katika kutekeleza ujumbe wa Mwenge wa mwaka huu.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa amesema, viongozi na watendaji wameonesha kwa dhati nia ya kuhifadhi Mazingira kwani miti 1513700 imepandwa ndani ya kipindi cha mwaka mmoja wa 2022/23 katika maeneo mbalimbali kama kwenye miradi ya maji.

"Hongereni sana Buchosa, ninyi ni mabingwa wa uhifadhi wa mazingira." amesisitiza kiongozi huyo wa Mbio za wmenge wa uhuru zinazoenda sambamba na kaulimbiu isemayo

"Tunza Mazingira, Okoa vyanzo vya Maji kwa Ustawi wa viumbe hai kwa Uchumi wa Taifa."

Akitoa taarifa ya mradi huo, kaimu mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Walter Njau amesema Halmashauri hiyo imejikita katika kutunza vyanzo vya maji, kurejesha uoto wa asili na Ikolojia ya viumbe hai na utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti ya aina mbalimbali ikiwemo ya matunda, miti ya mbao na miti ya asili.

Katika wakati mwingine, wakala wa maji na usafi wa mazingira Vijijini wilayani humo wameonesha nia ya kumtua mama ndoo kichwani wananchi zaidi ya 4118 kwa kuwaletea huduma ya maji safi kwa kuwajengea mradi wenye thamani ya zaidi ya milioni 190 ambao umewekewa jiwe la msingi (zaidi ya 85%) na Mwenge wa Uhuru ambao tayari umeshaanza kutoa maji.

Katika wakati mwingine, Halmashauri hiyo imedhihirisha shauku yao ya kutaka kuhifadhi vyanzo vya maji baada ya kuufikisha Mwenge kwenye mradi wa umwagiliaji unaolenga kuwanufaisha zaidi ya wakulima 700 kwa kupata chakula cha kutosha kabla ya kuzindua madarasa mawili Rwenchenga na kuweka mawe ya msingi kwenye bweni la wanafunzi Nyehunge.

Baada ya kushindwa kuzindua mradi wa jengo la huduma za dharula kwenye Hospitali ya wilaya kwa kukosa sifa za ubora na viwango stahiki kutokana na thamani ya fedha kiasi cha nilioni 300, Mwenge wa Uhuru umeiagiza Halmashauri ya Buchosa kujenga tabia ya kusimamia miradi vizuri ili iwe na tija kwa wananchi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti