• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Mwenge wa Uhuru waleta Hamasa Upatikanajia wa Maji,Ushiriki Uchaguzi Serikali za Mitaa

Posted on: May 14th, 2019

Mwenge wa Uhuru umeingia Mkoani Mwanza ukitokea Mkoa wa Shinyanga na Kupokelewa na Katibu Tawala Mkoa Christopher Kadio kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella tayari kukimbizwa Halmashauri zote za Mkoa wa Mwanza.

Huku kukiwa na hamasa ya kutosha, wananchi wa Mkoa wa Mwanza wamepokea Ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wa 2019 kwa furaha kubwa uliotolewa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa usemao "Maji ni Haki ya Kila Mtu, Tutunze Vyanzo vyake na Tukumbuke Kushiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa”.

Akitoa Taarifa ya Mkoa Kwa Niaba Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe John Mongella,Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Christopher Kadio amesema, Katika kuhakikisha Maji ni Haki ya Kila Mtu, Mkoa wetu, hadi Februari, 2019 upatikanaji wa huduma ya maji safi umeongezeka toka asilimia 55 iliyokuwepo Machi, 2018 hadi kufikai asilimia 59 Februari 2019 kwa wakazi wote wa Mkoa wa Mwanza. Kati ya hao, wananchi wanaoishi vijijini huduma ya maji safi imeongezeka toka asilimia 48 hadi asilimia 49, na kwa wananchi wanaoishi mjini, huduma ya maji safi imeongezeka kutoka asilimia 80 hadi asilimia 81.

Aidha, ameongeza kuwa, Ili kutekeleza adhma hii katika Mkoa wa Mwanza, Serikali imetekeleza miradi ipatayo 91 ikiwa; mijini ni miradi 8 na vijijini ni miradi 83. Miradiya vijijini ina vituo vya maji vipatavyo 1,243 vyenye thamani ya Tsh. Bilioni 233.3 na uwezo wa kuhudumia watu wapatao 989,155 toka mwaka2015. 

Aliongeza kuwa, mfano; Miradi 55 yenye thamani ya Tsh. 27.6 iliyo na vituo 875 yenye kuhudumia watu wapatao 437,500 imejengwa na kukamilika katika vijiji vya Halmashauri zote za Mkoa wa Mwanza. 

Pamoja na miradi hiyo ya vijijini, ipo na miradi mikubwa ya maji na usafi wa mazingira mijini iliyojengwa na kukamilika katika miji ya Nansio na Sengerema yenye thamani ya Tsh. Bilioni 37.2 inayohudumia wananchi wapato 218,000.

Hata hivyo, pamoja na kukamilisha kujenga miradi tajwa hapo awali, Serikali bado inaendelea na kujenga miradi mipya mingine ya maji ya bomba vijijini ipatayo 28 yenye jumla ya vituo vya maji 366 vyenye thamani ya tsh. Bilioni 37.2 ambayo itahudumia watu wapatao 183,000 vijijini.

 "Kwa upande wa mijini serikali inajenga miradi 4 yenye thamani ya Tsh. Bilioni 108.6 ikiwa ni ujenzi wa chanzo kipya cha maji Jijini Mwanza eneo la Butimba ambacho kitasambaza maji maeneo ya pembeni mwa Jiji yasiyokuwa na maji ya kutosha" alisema Kadio.

Aliendelea kuongeza kuwa, Uongozi wa Mkoa utaendelea kuhakikisha kwamba vyanzo vya maji vinatunzwa na kuhimiza  wananchi wa Mkoa wa huo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti