• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

OFISI YA MKUU WA MKOA ITAHAKIKISHA HAKI ZOTE ZA WATU WENYE ULEMAVU ZINALINDWA NA KUTEKELEZWA-RC MAKALLA

Posted on: July 6th, 2023

OFISI YA MKUU WA MKOA ITAHAKIKISHA HAKI ZOTE ZA WATU WENYE ULEMAVU ZINALINDWA NA KUTEKELEZWA-RC MAKALLA


*Awaahidi kutengewa maeneo ya biashara maeneo ya Masoko*


*Ashauri Mwanza kwenda kujifunza soko la Machinga Complex kuhusu kuwatengea vizimba watu wenye ulemavu*


*Usalama wao ndiyo kipaumbele cha kwanza*


*Ampongenza Mbunge wa viti Maalum Mhe. Khadija Shaaban kwa uwajibikaji mzuri kwa makundi maalum*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Amos Makalla amewakikishia watu wenye ulemavu Mkoani humo kuzilinda na kuzitekeleza haki zao zote wanazostahili kama watu wengine likiwemo kutengewa maeneo yao ya biashara kwenye Masoko na usalama wao kwa ujumla.

Amesema hayo leo wakati wa mazungumzo ya pamoja na wawakilishi wa Vyama vya watu wenye ulemavu na kula nao pamoja chakula kwenye ukumbi wa Mwanza Hotel ambapo amesisitiza hakuna nafasi ya mtu yoyote kubaguliwa kutokana na kasoro yake ya kimaumbile na wachache wanaofanya hivyo watambue mkondo wa sheria utawapitia.

"Nimekaa hapa nimewasikiliza wote mnaowawakilisha wenzenu changamoto zote mnazopitia,narudia kusema nimeyapokea na nitakwenda kuyafanyia kazi kasoro tu yale ya kisera na sheria,"CPA Makalla.

Amesema alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Da r-e.s-Salaam ametengeneza mazingira mazuri kwenye soko la Machinga Complex kwa kuwatengea maeneo rasmi watu wenye ulemavu, hivyo na kutaka Mkoa wa Mwanza ujifunze kwa mpango huo.

Mhe. Makalla amesema amesikia kilio cha Vyama hivyo kukosa Ofisi za kufanyika kazi hivyo suala hilo ameagiza litekelezwe haraka kwenye majengo yote ya Taasisi za Serikali wapatiwe nafasi.

"Tayari Rais wetu Dkt.Samia Suluhu ameshatoa maagizo hayo hivyo hakuna sababu ya kusua sua au kujadiliana wahusika wote mhakikishe viongozi hawa wa vyama vya walemavu wanapatiwa Ofisi za kufanyia shughuli zao,"amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Aidha amewatahadharisha wale wote wanaotoa lugha zisizo na staha kwa watu wenye ulemavu wakiwemo Albino kuwacha tabia hiyo na wanaowakataa kuingia kwenye vyombo vya usafiri LATRA na RTO wawachukulie hatua za kisheria

"Mhe.Mkuu wa Mkoa huu ni utaratibu niliojiwekea wa kuzunguka mikoani na kukutana na makundi maalum ninayoyawakilisha Bungeni,kusikiliza changamoto zao na kwenda kuzisemea ili ufumbuzi upatikane,"Khadija Shaaban maarufu kama Keisha,Mbunge wa viti maalum.

"Sisi kama wawakilishi wa wananchi tuna wajibu wa kupigania usawa wa wananchi wote,na kwa kupitia Mkutano huuu tunazidi kupata mengi ya kujifunza na kuyatekeleza," Mhe.Stanslaus Mabula,Mbunge wa Nyamagana.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti