• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Prof Mkenda ahitimisha ziara ya kikazi kanda ya ziwa, aridhishwa na utekelezaji wa miradi

Posted on: July 6th, 2023



Prof Mkenda ahitimisha ziara ya kikazi kanda ya ziwa, aridhishwa na utekelezaji wa miradi*


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Adolph Mkenda ameendelea na ziara ya siku tatu katika Mikoa ya kanda ya ziwa iliyojikita katika ukaguzi wa Miradi iliyo chini ya Wizara hiyo ambapo leo Julai 06, 2023 amefika Mkoani Mara akitokea Mkoani Mwanza.

Akizungumza na Uongozi na watumishi wa Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere cha Kilimo na Teknolojia kwenye Kampasi ya Oswald Mang'ombe, Prof Mkenda amesema amefurahishwa na Ukarabati wa Miundombinu ya chuo hicho ambao umeonesha nia ya dhati ya kutaka kudahili wanafunzi mwanzo wa muhula wa mwaka 2023/24.

"Tumezunguka kote, tumekagua na kwakweli tumeridhika na nina imani kwamba tukienda hivi basi tutakua tayari kupokea wanafunzi kwa ajili ya masomo ndani ya mwaka huu wa masomo na niwape tu taarifa kuwa tayari wajumbe wa baraza la Chuo wameshapatikana ambapo Mhe. Mizengo Pinda Waziri Mkuu Mstaafu ndiye Mkuu wa chuo hiki." amesema Prof Mkenda.

Amesema Serikali imeamua kutenga zaidi ya Bilioni 2.6 kwa ajili ya ukarabati huo ili kuinua Sekta ya Kilimo nchini na kwamba chuo hicho kitaleta alama isiyofutika kwenye mageuzi ya Kilimo na Teknolojia nchini na ametumia wasaa huo kutoa rai kwa Uongozi kuanza kwa vitivo vinavyobuniwa vizuri ili kutoa umahiri uliokusudiwa kwa vijana.

Akitoa salamu za Mkoa wa Mara, Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Said Mtanda ameihakikishia Wizara ya elimu ushirikiano ili kuhakikisha kinakarabatiwa na kuwa chuo cha mfano nchini ikiwa ni katika kuenzi pia tunu ya asili ya Baba wa Taifa Hayati Mzee Nyerere na kwamba kitakapokamilika kitachochea ubunifu, umahiri katika sekta ya kilimo na hata Utalii katika ukanda huo.

Mhe. Jumanne Sagini, Naibu Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi ametumia wasaa huo kuishukuru wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kuwaletea Butiama Miradi mbalimbali kwenye wilaya hiyo na ametoa rai kwa Uongozi wa Chuo hicho kuhakikisha Ukarabati unaanza mara moja na kukarabati chuo kwa ubunifu.

"Katika zoezi la Ukarabati Mhe. Waziri tumezishirikisha taasisi za wenzetu kama vile VETA, TBA, Bonde la Ziwa Victoria, Halmashauri ya wilaya ya Butiama na Ruwasa ambao wametuhakikishia kuwa tutapata maji ya kutosha kuhudumia chuo hiki." Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Lesakit Mellau


Naye, Prof. Msafiri Jackson ambaye ni Kaimu Mkuu wa Chuo Utawala, fedha na Mipango amebainisha kuwa Mradi wa Ujenzi wa Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Mwalimu Nyerere Kampasi ya Butiama utasaidia kuimarisha mafunzo ya kujifunzia na Ufundi Stadi.


Katika wakati mwingine Prof. Mkenda amefika  kwenye kijiji cha Rwamkoma na kukagua eneo Maalum ambalo itajengwa miundombinu ya Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Mwalimu Nyerere tawi la Butiama ambapo zaidi ya Bilioni 44.5 zitatumika chini ya Mradi wa Higher Education Econ. Trans (HEET) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti