• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

PROF. SHEMDOE ATAKA KUWEKWA MKAKATI WA KIMATAIFA KUDHIBITI UVUVI HARAMU ZIWA VICTORIA

Posted on: August 26th, 2024

PROF. SHEMDOE ATAKA KUWEKWA MKAKATI WA KIMATAIFA KUDHIBITI UVUVI HARAMU ZIWA VICTORIA


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe ametoa rai kwa Mataifa ya Kenya, Uganda na Tanzania, kufanya doria ya pamoja katika ziwa victoria, ili kukomesha uvuvi haramu na biashara ya mazao ya uvuvi, inayokiuka taratibu za kisheria ndani ya ziwa hilo.

Akifungua mkutano leo Agosti 26, 2024 wa kuhamasisha wadau wa uvuvi kudhibiti uvuvi haramu na biashara haramu ya mazao ya uvuvi ziwa victoria kwenye ukumbi wa mikutano Nyakahoja, Katibu Mkuu huyo amesema ziwa Viktoria linamchango wa asilimia 67% katika sekta ya uvuvi nchini, likiwa limeshuka kwa asilimia 17% kutoka 85%, likiwa na wavuvi 100,002, huku wanufaika wa moja kwa moja wa biashara ya mazao ya uvuvi wakiwa zaidi ya laki mbili.

"Serikali kwa kutambua mchango wa sekta hii inaendelea kuiboresha ikiwa pamoja na kutoa boti za kisasa na ukopeshaji bila riba kwa makundi maalum ya Ufugaji wa samaki wa vizimba".

Lakini Pamoja na mchango huo, kikwazo kikubwa kinacholikabili ziwa hili ni uvuvi haramu unaoangamiza mazalia ya rasilimali zilizopo ziwani humo". Amesisitiza Katibu Mkuu.

Aidha amewataka wadau wa sekta ya uvuvi kukaa na kuja na mikakati endelevu ya kimataifa ya kukomesha hali hiyo na kuiwasilisha Serikalini ili ifanyiwe maboresho mazuri na ziwa liendelee kuwa na tija kwa wananchi wa Mwanza na nchi jirani zinazozungukwa na ziwa hilo.

Kadhalika ameendela kwa kusema mradi wa uvuvi wa vizimba uliozinduliwa na Mhe. Rais mapema mwaka huu umekuwa na matokeo chanya na umeendelea kufanya vizuri, ambapo amesema wametoa boti 160 nchi nzima na 151 zimefanya vizuri.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Mohamed Sheikh, amesema hali ya uvuvi haramu imechangia uvunaji wa tani za samaki kushuka katika ziwa victoria, ukihusisha samaki aina ya sangara, dagaa, mabondo na mauzo kuporomoka.

"Wizara inakuja na mkakati wa kisasa wa kupambana na hali hiyo ukiwemo utumiaji wa ndege nyuki ili kuwabaini wanaojihusisha na uvuvi haramu na vifaa maalum vya ufuatiliaji". Amesema Prof. Sheikh

Akitoa Salamu za Mkoa kumuwakilisha Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Katibu Tawala Msaidizi, Uchumi na Uzalishaji, Bw. Emil Kasagara amesema viwanda vingi kwa sasa vinashindwa kujiendesha kwa ufanisi na vingine vikiyumba kutokana na upungufu wa rasilimali ziwa unaochangiwa na uvuvi haramu.

"Tumekuwa na vikao mbalimbali na wadau wa sekta hii kwa lengo la kuelimishana na kuhakikisha ziwa linaendelea kuwa kitega uchumi muhimu kwa wananchi" Kasagara.

Mkutano huo umewashirikisha Maafisa uvuvi kutoka Mwanza, Mikoa ya jirani na sekta binafsi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti