• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAIS SAMIA ATOA ZAIDI YA BILIONI 30 KUJENGA VIVUKO VIPYA MWANZA: RC MAKALLA

Posted on: January 10th, 2024

RAIS SAMIA ATOA ZAIDI YA BILIONI 30 KUJENGA VIVUKO VIPYA MWANZA: RC MAKALLA


*Amshukuru Mhe. Rais kwa kuboresha usafiri wa majini*


*Awataka TEMESA kumsimamia mkandarasi kukamilisha ujenzi*


*Awapongeza Songoro Marine kwa uhodari na kujenga boti za uokozi Ukerewe*


*Amezitaka Halmashauri kutatua changamoto za vituo vya ufuatiliaji*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo Januari 10, 2024 amekagua ujenzi wa vivuko vipya vitano vinavyojengwa kwenye karakana ya Songoro Marine Wilayani Ilemela kwa zaidi ya Bilioni 30.


Akiongea na uongozi wa mkandarasi huyo pamoja na wasimamizi (TEMESA) Makalla ametumia wasaa huo kumpongeza na kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha hizo kujenga vivuko vipya vitakavyoimarisha usafirishaji ziwani.

Amesema, awali wananchi waishio kwenye visiwa walipata shida kusafiri kwa kutumia mitumbwi jambo lililohatarisha usalama wao lakini kukamilika kwa vivuko hivyo kwa pamoja mwishoni mwa mwezi Machi 2024 kutaimarisha usafiri.


"Wananchi wetu siku za nyuma walitumia vivuko visivyo na uhakika, uwekezaji huu mkubwa wa Mhe. Rais wa zaidi ya Bilioni 30 kujenga vivuko hivi vipya utasaidia kuimarisha usafiri kwenye visiwa hususani Ukerewe, Magu na Sengerema." Mkuu wa Mkoa.

Aidha, amempongeza na kumshukuru mkandarasi Songoro Marine Co. Ltd kwa utekelezaji wa miradi hiyo kwa uaminifu na akawataka TEMESA kulipa fedha kwa wakati na kusimamia usiku na mchana ili kazi ikamailike kwa wakati kwa mujibu wa mkataba.


Awali, Mkurugenzi wa kampuni ya Songoro Marine Major Songoro ameahidi kujenga kwa kasi na kukamilisha kwa wakati kwa mujibu wa mkataba ili wananchi wanaovisubiri wapate uhakika wa usafiri kwenye maeneo na kwamba vyote kwa pamoja vitakamilika kabla ya mwezi Mei 2024.

"Mhe. Mkuu wa Mkoa tunaendelea na ujenzi wa vivuko vya Rugezi - Kisorya kwa zaidi ya Milioni 892, Ijinga -Kihangara kwa Bilioni 5, Bwiru -Bukondo kwa Milioni 677, Nyakalilo-Kome kwa zaidi ya Bilioni 8.5 pamoja na Buyagu-Mbariika kwa zaidi ya Bilioni 3.5 na tutakamilisha kwa mujibu wa mkataba." Mkuu wa Mkoa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti