• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAIS SAMIA AWATAKA WANANCHI WA MKOA WA MWANZA KUTANGULIZA UZALENDO NA KUILINDA MIRADI

Posted on: June 14th, 2023

RAIS SAMIA AWATAKA WANANCHI WA MKOA WA MWANZA KUTANGULIZA UZALENDO NA KUILINDA MIRADI


*Amtaka Mtendaji Mkuu TANROADS kulisimamia kikamilifu liwe na ubora*


*Awahakikishia wananchi kasi ya kuwaletea Maendeleo*


*Ashukuru kwa mapokezi makubwa tangu amewasili Mwanza*


*Aahidi kukuza uchumi Watanzania  kwa kupitia miradi *


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka wananchi wa Mkoa wa Mwanza kutanguliza uzalendo katika mradi ya maendeleo na kuepukana na aina yoyote ya wizi ambao utarudisha nyuma kasi ya umaliziaji wake.

Akizungumza leo na wananchi Wilayani Misungwi mara baada ya kupata taarifa ya mradi wa Daraja la Kigongo- Busisi, Dkt.Samia amesema huo unakuja kukuza uchumi wa Taifa na wananchi wa eneo hilo hivyo wana kila sababu ya kuulinda kwa faida yao.

"Ndugu zangu wananchi nimepita kidogo hapa kuona maendeleo ya mradi huu ambao sasa umefikia zaidi ya asilimia 70 kabla ya kukamilika,nimefarijika ila nimesikia kuna ka-mkono wa udokozi wa vifaa,kemeeni hilo na wacheni," amesisitiza Mhe.Rais.

Aidha, amemtaka Mtendaji Mkuu wa wakala wa barabara TANROADS, Mhandisi Mohamed Besta kuhakikisha Daraja hilo linakuwa na ubora kwa kusimamia kila hatua na vipimo vyote vifanywe kwenye maabara za Serikali na siyo kufanywa na Mkandarasi pekee.

"Mhe.Rais Daraja hili linalojulikana kama JP Magufuli lenye urefu wa kilomita 3 limegharimu Shs bilioni 716.33 na hadi sasa Mkandarasi CCECC Construction kutoka China amelipwa Shs bilioni 368.67 na tumefikia asilimia 75 ya utekelezaji na itapitiwa na barabara kuu ya Usagara-Sengerema hadi Geita,"  Mhandisi Besta

Mtendaji huyo Mkuu wa wakala wa barabara nchini amebainisha mradi huo wa Daraja pia umekuwa ni darasa kwa wahandisi wa hapa nchini kutokana na kuwekwa katika kila eneo kwa lengo la kuongezewa ujuzi.

"Mhe.Dkt.Samia kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Misungwi tunaendelea kukushukuru kwa kuonesha kwa vitendo kasi ya maendeleo,miradi mingi imefanyika Jimboni kwangu kuanzia Sekta ya afya na elimu,na wananchi wa Misungwi wamefurahi sana kutujengea barabara ya Mwanangwa hadi Misasi kwa kiwango cha lami",Mhe.Alexander Mnyeti,Mbunge wa Misungwi

Akikagua Ujenzi wa Meli ya MV Mwanza inayojengwa kwa Bilioni 109 kwenye Bandari ya Mwanza Kusini Mhe. Rais amewataka watanzania kufanya kazi kwa bidii ili ukamilifu wa Meli hiyo inayotarajia kubeba zaidi ya Watu 1200 na Tani 400 za Mizigo kwa wakati mmoja usaidie kufungua uchumi wa nchi kwa kubeba mizigo.

"Tunakwenda kuwafungua watanzania kiuchumi, tunajenga Meli, Bandari na Reli viende sambasamba na sisi kufanya kazi kwa bidii ili kila kinachozalishwa kwenye mashamba yetu kiende sokoni na kazi hii inafanywa kwenye kila kona ya nchi hii," Amesisitiza Rais Samia.


Naye, Mkurugenzi wa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) Erick Hamissi amesema meli hiyo imeshajengwa kwa zaidi ya asilimia 80 na kwamba mkandarasi ameshalipwa fedha hadi hatua hiyo na inatarajiwa kukamilika Mwezi Agosti 2023 na watanzania zaidi ya 200 wameajiriwa hapo wakiongozwa na wataalamu Wakorea 13 tu.

Katika wakati mwingine, Mhe. Rais  amewapongeza NSSF kwa Mradi mzuri wa Hoteli ya Kisasa ambayo italeta Tija mkoani humo na akawataka kupanua huduma hiyo kwenye majiji mengine Nchini.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti