• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAS BALANDYA AAHIDI USHIRIKIANO ZAIDI NA JIJI LA WURZBURG- UJERUMANI

Posted on: November 8th, 2024

RAS BALANDYA AAHIDI USHIRIKIANO ZAIDI NA JIJI LA WURZBURG- UJERUMANI


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndg. Balandya Elikana amewapokea waheshimiwa Madiwani na watendaji kutoka Halmashauri ya Jiji la Wurzburg- Ujerumani na kuwahakikishia ushirikiano zaidi na Jiji la Mwanza kwa faida ya wananchi wa pande zote mbili.

Akizungumza na wageni hao Ofisini kwake mapema leo asubuhi Novemba 08, 2024 mtendaji huyo wa Mkoa amebainisha Jiji la Wurz burg limekuwa na miradi mingi ya kijamii Jijini Mwanza yenye lengo la kuwaletea maendeleo wananchi hivyo hakuna budi kuudumisha ushirikiano huo.

"Tunatambua baadhi ya miradi inayofadhiliwa na Jiji la Wurzburg ikiwemo mradi maji safi huko kisiwa cha Ijinga wilayani Magu, vifaa tiba na mafunzo kwa wataalamu wa afya kwenye hospitali ya Nyamagana, uwekaji wa umeme wa mwanga wa jua kwenye jengo la Halmashauri ya Jiji la Mwanza na ujenzi wa madarasa na maktaba shule ya msingi Butimba hii ni miradi yenye kuwaletea tija ya maendeleo wananchi",Balandya.

Aidha amesema Serikali ya Mkoa wa Mwanza inazidi kupiga hatua ya kuwaondelea umasikini wananchi wake kwa kuwawezesha miradi mbalimbali ukiwemo ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba kwa kupitia mikopo isiyo na riba.

Kiongozi wa msafara huo uliowajumuisha Madiwani na Meya,Bi Babra Lehrieder amemshukuru mwenyeji wake kwa mapokezi mazuri na kubainisha lengo la ujio wao ni kujionea miradi hiyo na kuhakikisha inazidi kuwa na ustawi mzuri kwa wananchi hali itakayoleta maana zaidi ya ushirikiano baina ya majiji hayo.

Katika ziara hiyo Madiwani hao wataitembelea pia nyumba ya kihistoria ya Gunzet house iliyopo katikati ya Jiji la Mwanza ambayo ilijengwa na wakoloni wa kijerumani kwa lengo la kujihami na adui ambayo awali waliifanyia ukarabati wa zaidi ya shs milioni 200 ili iwe na mvuto zaidi wa kitalii kama eneo la makumbusho.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti