• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAS BALANDYA AHIMIZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO H/ZA BUCHOSA NA SENGEREMA

Posted on: June 26th, 2024

RAS BALANDYA AHIMIZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO H/ZA BUCHOSA NA SENGEREMA


Halmashauri za Buchosa na Sengerema zimehimizwa kuwa na kasi ya ukusanyaji wa mapato ya ndani ili wazidi kuboresha huduma kwa wananchi na kupangilia mipango ya maendeleo kwa uhakika.

Rai hiyo imetolewa leo Juni 26,2024 kwa nyakati tofauti kwenye halmashauri hizo na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw Balandya Elikana wakati wa vikao vya Baraza la Madiwani kujadili  hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali,CAG za mwaka wa Fedha 2022-23,amesema Halmashauri hizo zikiweka mkakati mzuri wa ukusanyaji mapato tija ya maendeleo kwa wananchi itazidi kuimarika.

"Nimesikia mlivyovuka malengo yenu ya ukusanyaji mapato hapa Buchosa kwa kuvuka zaidi ya asilimia 100,hongereni sana sasa ongezeni bidii kuanzia sasa ili muweze kuwa na miradi mingi ya kuwaletea maendeleo wananchi,"Balandya

Mtendaji huyo wa Mkoa amewataka pia Madiwani wa Halmashauri hiyo kusimamia vyema miradi ya maendeleo na kutoruhusi hoja za CAG kujirudia.

"Halmashauri ya Buchosa katika ukaguzi wa Hesabu za CAG mwaka 2022-23 walikuwa na hoja 6,tano za zamani na moja ya 2022-23 ambayo ipo katika utekelezaji,"Laban Kilulu,Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu Serikali

Akiwa kwenye halmashauri ya Sengerema iliyofikisha asilimia 86 ya mapato yake ya ndani Balandya ametoa maagizo ya kuhakikisha hoja zote zikamilishwe kwa wakati.

"Hesabu za CAG zinaonesha mmepata hati safi kwa miaka mitatu mfululizo na mlikuwa na hoja 17 na 16 mmezikamilisha na kubakiza 4 za nyuma ambazo nataka zikamilishwe,"Mtendaji wa Mkoa

Kuhusu madeni ya wazabuni ya zaidi ya milioni 400 amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Sengerema kuongeza bajeti ya kuwalipa ili waweze kumudu shughuli zao

"Haiwezekani Mkurugenzi ukatenga milioni 50 ya kuwalipa wazabuni ni dhahiri utawapa umasikini kwa kushindwa kuwalipa kwa muda mrefu",amesisitiza Balandya

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe.Senyi Ngaga amebainisha maagizo yote yaliyotolewa watayafanyia kazi na hasa ukusanyaji mapato ya ndani.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti