• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAS Balandya ashauri Asasi za kiraia kushikamana kuelimisha jamii kutokomeza ukatili wa kijinsia

Posted on: December 2nd, 2023

RAS Balandya ashauri Asasi za kiraia kushikamana kuelimisha jamii kutokomeza ukatili wa kijinsia


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndg. Balandya Elikana amezishauri Asasi za kiraia kushirikiana kwa pamoja katika kuongeza kasi ya uelimishaji kwa jamii kuhusiana na ukatili wa kijinsia huku wahanga wakubwa wakiwa ni watoto, wasichana na wanawake.

Akizungumza leo katika Maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kwenye ukumbi wa mikutano wa M 14 uliopo chuo kikuu cha Mt. Agustino, Mtendaji huyo wa Mkoa amebainisha licha ya sheria za kupambana na hali hiyo kuwepo ikiwemo Ile ya Maudhui mtandaoni 2020 bado vitendo vya ukatili wa kijinsia vimekuwa vikifanyika.

"Wahanga wengi wamekuwa wakinyamazia vitendo hivyo kwa hofu na kuamini kuwa watadhalilika zaidi endapo suala lake litafikishwa kwenye vyombo vya sheria", amefafanua Balandya wakati akizungumza na washiriki wa Maadhimisho hayo wengi wakiwa ni mawakili na wanachuo wanaosomea sheria.

Balandya amezipongeza Asasi hizo za kiraia kwa kushirikiana na Serikali kwa kupunguza vitendo hivyo kwani takwimu zimeonesha mwaka 2016 ilikuwa asilimia 60 na mwaka 2022 asilimia 47.

"Ndugu mgeni rasmi kwa kutambua umuhimu wa jamii kuelimika hasa uhuru uliopo sasa mitandaoni,mahakama itaendelea kutoa elimu na kuepuka aina yoyote ya hofu kwa wahanga",Mhe. Stanley Kamanya,Jaji Mfawidhi Kanda ya Mwanza.

"Kuongezeka kwa matumizi ya Teknolojia ni dhahiri wahanga wakubwa wamekuwa ni wasichana na wanawake na madhara yake ni kushindwa kushiriki kikamilifu katika masuala ya kiuchumi na kugubikwa na msongo wa mawazo na mwishowe baadhi yao kuchukua maamuzi mabaya ya kujiua,"Mhe.Lilian Temba,Jaji wa Mahakama kuu Kanda ya Mwanza.

Kwa upande wake Mhadhiri wa Saut,Dkt.Neema Mwita aliyemwakilisha Makamu Mkuu wa chuo amebainisha Saut imekuwa na mchango mkubwa  kwa kuwatoa wataalamu wa sheria ambao wamekuwa  chachu ya kutoa msaada wa kisheria kwa jamii.

Katika Maadhimisho hayo washiriki wamepata wasaa wa kuona mfano wa Mahakama zinavyo fanya kazi katika kuendesha kesi za ukatili wa kijinsia.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti