• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAS BALANDYA AWAKARIBISHA VIONGOZI WA PPRA MWANZA

Posted on: June 18th, 2024

RAS BALANDYA AWAKARIBISHA VIONGOZI WA PPRA MWANZA


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana leo Juni 18, 2024 amewapokea na kufanya nao mazungumzo Mkoani Mwanza Bodi ya Wakurugenzi na Menejimenti kutoka Mamlaka ya Udhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA) ambao wako Mkoani humo kwa ziara ya kikazi ya kukagua na kutembelea miradi ya kimkakati inayotekelezwa.

Balandya amesema kama Viongozi wa Mkoa wanatambua mchango mkubwa unaofanywa na PPRA katika nchi kwa kuzingatia kuwa takribani 80% ya bajeti ya Serikali ni ununuzi wa umma.

Aidha  ameipongeza Bodi na Menejimenti hiyo kwa usimamizi mzuri wa mfumo wa usimamizi wa Ununuzi wa Umma Kielektroniki (Nest), kwani umesaidia na kuongeza uwazi pamoja na uwajibikaji.

"Shughuli zote za manunuzi ya umma zinafanyika kupitia mfumo huu wa Nest, nina imani tukiendelea kuutumia italeta mapinduzi makubwa katika sekta nzima ya manunuzi ya umma".

Kadhalika Mtendaji huyo wa Mkoa ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia kwa kuendeleza miradi yote mikubwa ya kimkakati katika Mkoa wa Mwanza, pia ameishukuru PPRA kwa kukubali kufanya na kuidhinisha manunuzi katika miradi yote hiyo ikiwemo mradi wa daraja la Kigongo-Busisi, Soko la Kisasa lililopo mjini kati, ujenzi wa Meli ya MV. Mwanza Hapa Kazi Tu, na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza

Naye Mkurugenzi Mkuu wa PPRA Bw. Eliakim Maswi amesema kwa sasa wana sheria mpya wanayoitumia ambapo Serikali imeamua kuwapa kipaumbele makampuni ya ndani katika kusimamia na kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati na maendeleo ikiwa na adhma ya kuhakikisha kuwa inayalea makampuni ya ndani.

"Kwa sheria yetu hii mpya, sasa siyo kila miradi mikubwa wapewe watu au makampuni kutoka nje, tunataka pia makampuni ya ndani yakue, mabadiliko makubwa yamefanyika chini ya Rais wetu Dkt. Samia na yataleta tija katika kuyakuza makampuni yetu ya ndani". Amesema Maswi.

Wakati huo huo Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw.Balandya Elikana mapema leo Ofisini kwake amefanya mazungumzo na Makamanda kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ambao wapo Mkoani humo kwa maandalizi ya sherehe za uvulishwaji nishani kwa Maofisa wake na askari siku ya kesho

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti