• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAS BALANDYA AWAPONGEZA ICAP KWA USHIRIKIANO NA SERIKALI YA MKOA WA MWANZA

Posted on: November 12th, 2024

RAS BALANDYA AWAPONGEZA ICAP KWA USHIRIKIANO NA SERIKALI YA MKOA WA MWANZA


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bwana Balandya Elikana leo Novemba 12, amewapokea na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Shirika lisilo la Kiserikali la ICAP kutoka nchini Marekani na kuwashukuru kwa kuendelea kuiunga mkono Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkoa wa Mwanza kwa kuwezesha ajira zaidi ya wafanyakazi 400 katika sekta ya afya.

Akizungumza mara baada ya kuwapokea, Katibu Tawala amewashukuru Viongozi hao ambao ni Mkurugenzi wa Fedha wa ICAP kutoka Makao Makuu New York, Marekani, Bibi Amy Gustavsson, ambaye aliambatana na Naibu Mkurugenzi Mkazi wa ICAP Tanzania, Dkt. John Kahemele pamoja na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa shirika hilo nchini, Ndugu Godfrey Hoya kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali za kuboresha kinga dhidi ya kuzuia na matibabu ya Virusi vya UKIMWI Mkoani Mwanza.


Aidha Bwana Balandya amewashukuru kwa kuendelea kuhamasisha kutahiriwa kwa wanaume kwa hiari kati ya vijana wenye umri kuanzia miaka 18 mpaka 29, na ameshuhudia idadi kubwa ya vijana wakijitokeza kuhudhuria kliniki hiyo ambayo imekuwa na umuhimu mkubwa katika kupunguza maambukizi na kusambaa kwa virusi vya UKIMWI.

"Ninaendelea kuwashukuru kwani kupitia ICAP, Tumeongeza idadi ya wahudumu wa afya katika vituo vya afya ili kuhakikisha tuna rasilimali watu na tunafanikiwa kutoa huduma bora za afya kwa wananchi".


Kadhalika amesema ushirikiano wa ICAP umesaidia katika ufungaji wa nishati ya jua kwenye vituo vya afya 81, hali iliyopelekea kuwepo kwa usambazaji wa umeme wa uhakika na huduma kutolewa bila adha ya nishati muhimu ya umeme.

Kwa upande wake, Bibi Amy amemshukuru Katibu Tawala na Serikali ya Tanzania kwa ujumla kwa ushirikiano mkubwa ambao ICAP imekuwa ikiupata na ameahidi kuendelea kushirikiana na Mkoa wa Mwanza na Tanzania kwa ujumla ili kuboresha afya za wananchi na kufikia malengo ya kuimarisha huduma za afya nchini.

ICAP ni Shirika lililo chini ya Chuo Kikuu cha Columbia, linaendesha miradi mbalimbali ya afya Mkoani Mwanza inayolenga kupambana na UKIMWI na kifua kikuu kwa ufadhili wa serikali ya Marekani kupitia PEPFAR na CDC.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti