• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAS Mwanza ashauri ufugaji wa kisasa wa Samaki wa vizimba ufanyike kwa awamu ziwani

Posted on: January 11th, 2024

RAS Mwanza ashauri ufugaji wa kisasa wa Samaki wa vizimba ufanyike kwa awamu ziwani


Leo Januari 11, 2024 Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana ameupokea ugeni Ofisini kwake kutoka Wizara ya mifugo na uvuvi ukiongozwa na Afisa Uvuvi Mkuu Bi. Mkonanile Mahundi.

Katika mazungumzo yao mafupi, Balandya ameipongeza Wizara hiyo kwa mkakati wenye tija wa kuwajengea uwezo vijana wa kujiajiri na kushauri mpango huo wa ufugaji kwa njia ya vizimba ufanyike kwa awamu kutokana na wingi wa vikundi husika kutoka mikoa ya kanda ya ziwa.

"Serikali ya Rais Samia imedhamiria kuwainua kundi la vijana kimaendeleo, mpango huu wa ufugaji wa kisasa wa samaki wataalamu kutoka wizarani ukiwawekea mazingira mazuri ya kazi utazidi kuwa na tija kwao kiuchumi", amefafanua Mtendaji huyo wa Mkoa wakati wa mazungumzo hayo.

Ameitaka Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuweka ushirikiano na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ili kuhakikisha miradi hiyo inafanyiwa ufuatiliaji na kuwa endelevu na mwishowe inafikisha ndoto ya Rais Samia kuona inawakomboa kiuchumi vijana.

Kwa upande wake Afisa Uvuvi Mkuu Bi. Mkomanile Mahundi amesema lengo la kuja Mwanza ni kukagua mchakato mzima wa mradi huo ikiwemo kukagua andiko la mkopo la mradi kutoka vikundi husika na kushauri pale zitakapo bainika changamoto ili zoezi hilo liwe limekamilika kabla ya Januari 29 2024.


"Tutapita maeneo yote Mikoa ya Kanda ya Ziwa ambayo mradi huu wa ufugaji wa samaki kisasa kwa njia ya vizimba unafanyika ili tujiridhishe kwa kila hatua kabla ya kuwakabidhi wahusika wote waliokidhi vigezo vya mradi huu",amesisitiza Bi.Mahundi

Mkoa wa Mwanza una jumla ya vikundi 79 wakiwemo watu binafsi 11, kampuni 6, vijana 13 na vikundi 49 huku Serikali ikiwa imetoa jumla ya Bilioni 65 kufanikisha mradi huo wa ufugaji samaki kwa njia ya vizimba ukiwemo pia kuwapatia wavuvi boti za kisasa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti