• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAS Mwanza ataka Jamii kuelimishwa zaidi kuhusiana na maambukizi dhidi ya Virusi vya Ukimwi

Posted on: June 2nd, 2022

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ngusa Samike ametoa rai kwa viongozi na watendaji mkoani humo kutoa elimu ya matumizi sahihi na usambazaji wa Makasha ya Kondomu kwa jamii ili kujikinga na maambukizi ya Ukimwi.


Akizungumza kwa niaba yake,Katibu Tawala Msaidizi Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji Mkoani Mwanza Emil Kasagara amesema hayo leo wakati akifungua kikao kazi cha Usambazaji wa Mkakati na Mwongozo wa Taifa wa Kondomu kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa watendaji wa mitaa kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela na Jiji la Mwanza.

"Niwaombe tukafikishe elimu hii kwa jamii, hakikisheni tunatoka na majibu ya namna gani kondomu zitawafikia wananchi wote maana sifa yetu Mwanza ni kufanya vizuri kwa hiyo twende tukashirikiane kuhakikisha kondomu zinawafikia maeneo ya vijijini. "

 "Lengo la kuwa hapa nanyi ni kuwajengea uwezo ili kuhakikisha kondomu zinafika kwenye jamii na tunatoa elimu ya matumizi sahihi, hivyo Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya waziri Mkuu tunahakikisha malengo hayo yanatimia." amesema Dktr. Emmanuel Mihayo, Mratibu wa kondomu Wizara ya Afya (NACP)

Mratibu wa Kondomu kutoka TACAIDS Dktr Hafidh Ameir amesema mpango huu ni kwa Mikoa 8 ambayo imeonesha inahitaji mkazo wa elimu hiyo na mpango wa kuzungukia nchi nzima utafanyika.

"Wengine wanapuuzia wakidhani UKIMWI haupo lakini ni vizuri wana semina tukasikiliza kwa makini ili tukatoe elimu kwa wananchi dhidi ya janga hili ambalo kwa muda mrefu halina tiba." Amesema, Naibu Meya wa Jiji la Mwanza Mhe. Rodrick Ngoye.


Kikao kazi hicho kinafanyika kwa siku mbili lengo likiwa ni kuwajengea uwezo Wataalam wa Sekta ya Afya, Watendaji wa Serikali za Mitaa pamoja na Madiwani kutoka Wilaya za Nyamagana na Ilemela kupambana na ugonjwa wa Ukimwi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti