• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAS Mwanza atoa rai kwa Wahandisi kusimamia Ubora wa Miradi

Posted on: August 22nd, 2023

RAS Mwanza atoa rai kwa Wahandisi kusimamia Ubora wa Miradi


Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndugu Daniel Machunda amewasihi Wahandisi kusimamia taaluma yao vema na  kutekeleza miradi katika ubora unaokusudiwa.

Ametoa wito huo leo Agosti 22, 2023 kwenye Kikao kazi cha Wahandisi, Maafisa Elimu na Waganga Wakuu wa Wilaya kilichoketi kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kufanya tathmini ya changamoto zinazowakabili kwenye utekelezaji wa miradi.

Machunda amesema serikali inatoa fedha nyingi kwa ajili ya kujenga Miundombinu na kuwaboreshea wananchi huduma hivyo ni wajibu wa wataalamu kusimamia ubora na thamani ya fedha kwenye utekelezaji.

"Twendeni tukajenge miradi iliyo bora, ni lazima tujenge Imani kwa wananchi kwamba serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia ipo kwa ajili ya kuwapa huduma bora sio tunajenga mradi mwaka huu alafu baada ya miaka michache mradi unaharibika." Machunda amefafanua.

Naye Katibu Tawala Msaidizi Seksheni ya Miundombinu, Mbunifu Majengo Chagu Nghoma amefafanua kuwa kikao kazi hicho kimelenga kufanya tathmini ya miradi iliyotekelezwa kwenye mwaka 2022/23 ambapo wameziangazia changamoto walizopitia na kwa pamoja wamebaini namna bora ya kutekeleza kwa siku za usoni.

Aidha, amebainisha kuwa kwa pamoja wamekubaliana kutekeleza miradi kwa ushirikiano ili kuhakikisha Wahandisi na idara watumiaji wanakuwa sehemu ya utekelezaji na kuitunza miradi kwa faida ya vizazi vya sasa na miaka ya baadae.

Vilevile, mbunifu majengo Nghoma amefafanua kuwa kwenye kikao kazi hicho wameihusisha Ofisi ya TAKUKURU ambayo imetoa wito kwa wataalamu hao kuwa wazalendo kwa kuzingatia kunakua na thamani ya fedha iliyokusudiwa kwenye miradi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti