• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAS MWANZA AZINDUA BODI YA USHAURI YA MWACHAS

Posted on: April 3rd, 2025

RAS MWANZA AZINDUA BODI YA USHAURI YA MWACHAS


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza  Ndg.Balandya Elikana leo Aprili 3,2025 amezindua rasmi Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi Mwanza (MWACHAS) huku akitoa wito kwa uongozi wa chuo na wadau wa elimu kushirikiana katika kuboresha sekta ya afya kupitia mafunzo bora kwa wanafunzi.

Akizungumza wakati wakati wa uzinduzi huo uliofanyika chuoni hapo eneo la Bugando wilayani Nyamagana, Balandya ameipongeza MWACHAS kwa hatua yake ya kuunda bodi imara ya ushauri akisisitiza kuwa taasisi za elimu zina jukumu kubwa la kuandaa wataalamu wa afya watakaosaidia kuboresha huduma za tiba nchini.

"Tunahitaji kuhakikisha kuwa vyuo vya afya vinakuwa na mifumo madhubuti ya kusimamia ubora wa elimu na mafunzo ili kuzalisha wahitimu wenye weledi wa hali ya juu,"Katibu Tawala

Aidha, ameitaka bodi hiyo kushirikiana na Serikali pamoja na wadau wengine ili kutatua changamoto zinazokabili chuo, hususan katika upatikanaji wa miundombinu bora.

 "Serikali iko tayari kushirikiana nanyi lakini ni lazima kuwe na mipango thabiti ya maendeleo ili MWACHAS iwe chuo bora kinachotoa mafunzo yenye viwango vya kimataifa".amesisitiza mtendaji huyo wa mkoa

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi hiyo Bw.Isaaka Ndasa amesisitiza kuwa jukumu kuu la bodi hiyo ni kuhakikisha MWACHAS inazidi kupiga hatua na kuwa miongoni mwa taasisi za elimu ya afya zinazoongoza nchini.

 "Tutahakikisha tunasimama imara ili kuboresha viwango vya elimu, kufuatilia mwenendo wa chuo na kuhakikisha kwamba chuo chetu kinaendelea kukua",Ndasa


Mwenyekiti huyo pia ametoa wito kwa wanachama wa bodi hiyo kufanya kazi kwa bidii na ushirikiano ili kutimiza malengo ya chuo.

Mkuu wa Chuo, Prof.Hyasinta Jaka ambaye pia ni Katibu wa Bodi hiyo ameiomba Serikali kusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili chuo hicho hasa katika eneo la ujenzi wa Chuo katika eneo lililopo karibu na Hospitali ya Wilaya ya Ilemela Mwanza.

Aidha amesisitiza kuwa chuo kina dhamira ya kutoa elimu bora kwa wanafunzi wake, lakini kinahitaji msaada zaidi ili kuboresha vitendea kazi na kuongeza idadi ya wahadhiri wenye uzoefu.

Uzinduzi huo umehudhuriwa na viongozi wa Serikali, wadau wa elimu, wahadhiri, na wanafunzi wa MWACHAS.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti