• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAS MWANZA AZITAKA HALMASHAURI KUTENGA FEDHA KUSIMAMIA MPANGO WA M-MAMA

Posted on: August 17th, 2024

RAS MWANZA AZITAKA HALMASHAURI KUTENGA FEDHA KUSIMAMIA MPANGO WA M-MAMA


Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Daniel Machunda amezitaka Halmashauri zote za Mkoa huo kutenga bajeti za kutekeleza mpango wa M-Mama unaotekeleza rufaa kwa ajili ya matibabu kwa wajawazito, waliojifungua na watoto ili kukomesha vifo vitonanavyo na uzazi.

Bwana Machunda ametoa wito huo mapema leo Agosti 17, 2024 wakati akifungua kikao kazi cha kujadili uendelevu wa mfumo wa usafirishaji wa wajawazito, waliojifungua na watoto kwenda kupata huduma za afya M- Mama katika hoteli ya Adden Palace Ilemela.

Aidha, ameagiza vituo vya afya kuweka mikakati thabiti ya upokeaji wa rufaa na  waratibu wa zoezi hilo kusimamia kwa weledi na wakati ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya wakati wote na kuhakikisha Taifa linakua na uzazi salama wakati wote.

"Vifo vitokanavyo na uzazi vinaumiza sana, ni lazima tuhakikishe kujifungua kunakua ni neema na sio janga kwa jamii kwani ni jambo la neema tulilopewa na Mwenyezi Mungu", amesisitiza ndugu Machunda ambaye ni Katibu Tawala Msaidi sehemu ya Utawala na Usimamizi wa rasilimali watu.

Naye, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Jesca Lebba amesema mfumo wa usafirishaji wa dharula kwa wajawazito, waliojifungua pamoja na watoto una miezi 18 tangu kutambulishwa Mwanza na rufaa zilianza kwa kupiga namba 115 na kwamba Serikali imeshirikiana na wadau wakati wote kufanikisha rufaa.

Aidha, amesema pamoja na majukumu mengine waratibu wamekagua na kuweka vifaa kwenye uratibu wa kituo cha kupokelea wagonjwa cha hospitali ya rufaa ya Mkoa Sekou Toure na kwamba rufaa 4775 zimefanyika na Jumla ya Milioni 14.4 zimechangwa kwenye akaunti ya Taifa.

Meneja wa kanda wa shirika la Pathfinder Charles Kato amesema kuwa wanayo furaha kukabidhi majukumu ya utekelezaji wa usafiri wa dharula kwa wajawazito, waliojifungua pamoja na watoto na kwamba wataendelea kushirikiana na Serikali katika kushauri masuala mbalimbali.

Vilevile, Meneja huyo amebainisha kwamba wahisani wote awali walijipanga kuihudumia mikoa yote ya Tanzania hadi 2027 kwa kushirikiana na Serikali na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan aliagiza ifikapo Oktoba 2024 wahakikishe wamefika kote na kukabidhi majukumu kwa watendaji wa Serikali ili kujenga tabia ya kujitegemea.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti