• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AAGIZA KUANZA MARA MOJA KWA UJENZI WA BARABARA YA SENGEREMA-BUCHOSA

Posted on: November 8th, 2023

RC MAKALLA AAGIZA KUANZA MARA MOJA KWA UJENZI WA BARABARA YA SENGEREMA-BUCHOSA


*Awataka TANROADS kumpatia Mkandarasi maeneo yasiyo na mgogoro waanze kujenga mara moja*


*Aiagiza Halmashauri ya Sengerema kuhakiki madai ya wananchi wenye Ofa na Hati kwenye mradi huo*


*Aitaka Halmashauri kuweka vipaumbele kwenye Mapato ili kuwe na mpango wa ulipaji wa madeni mbalimbali*


*Aagiza utatuzi wa migogoro kwa haraka ili kudhibiti uvunjifu wa amani kwenye familia*


*Awataka watendaji ngazi za Kata na Vijiji kutenga siku kwenye wiki kusikiliza kero hususani za ardhi na kuzimaliza*


*Auagiza uongozi wa Wilaya na Halmashauri kutathmini Madai ya fidia kwenye ujenzi wa stendi*


*Ataka kutekelezwa kwa maagizo yote aliyoagiza ndani ya siku 14 na apate taarifa ya utekelezaji wake*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe CPA Amos Makalla amemtaka Mkandarasi AVM-Dilingham anayejenga barabara ya Sengerema- Buchosa yenye urefu wa Kilomita 54.4 kwa gharama ya zaidi ya Bilioni 73 kuanza mara moja ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami kwa mujibu wa Mkataba.

Ametoa agizo hilo leo Novemba 08, 2023 wakati wa usikilizaji na utatuzi wa kero za wananchi kwenye mkutano uliofanyika kwa zaidi ya saa 11 kwenye Stendi ya zamani ya Mabasi Sengerema na kubaini kuwa tangia mkataba usainiwe mwezi Aprili ujenzi haujaanza huku zikitajwa sababu mbalimbali.

Mhe. Makalla amesema haiwezekani mkataba wa ujenzi wa mradi huo usainiwe mwezi aprili lakini hadi sasa ujenzi wake usianze tena kwa sababu za kizembe wakati Mhe. Rais ameridhia kujengwa kwa barabara hiyo na fedha ameshatoa.

"Ninawaagiza TANROADS mhakikishe mkandarasi anaanza ujenzi wa hii barabara mara moja hususani kwenye maeneo ambayo hayahitaji kufidia ardhi, Serikali imeridhia kujenga barabara hii sasa kwanini tunachelewa ujenzi huu ambao wananchi wameisubiri kwa muda mrefu." Makalla amesisitiza.

Aidha CPA Makalla ameitaka halmashauri ya Sengerema kuhakiki madai ya wananchi wanaodai kuchukuliwa maeneo yao kupisha ujenzi huo ili ibainike nani ana ofa au Hati na uhalali wake ili gharama stahiki zifahamike na kulipwa mara moja na ujenzi uendelee.

"Wakati tunashughulikia eneo lenye mgogoro nawaagiza Halmashauri ihakiki eneo lenye ofa au Hati za kisheria ili tujue gharama na mniletee taarifa ili tutangaze kuwa eneo fulani lina mgogoro kutokana na wananchi kupewa Hati kwenye eneo la barabara", Mkuu wa Mkoa.

Kutokana na kukithiri kwa kero za ardhi, Makalla amewaagiza watendaji kuanzia ngazi za vijiji na Kata kutenga siku maalum ndani ya juma kusikiliza na kutatua kero za wananchi ili kuwajengea Imani na Serikali ya Rais Samia ambayo imejipambanua kwenye kuhudumia wananchi wakati wote.

"Punguzeni matatizo na kero za ardhi kwa wakati kwani kuongezeka kwa kero kwenye eneo fulani sio sifa nzuri hususani kwenye sekta moja,  hapa leo zaidi ya asilimia 90 ya kero zilizowasilishwa ni za ardhi sasa maana yake ni kwamba idara hii na watendaji hawafanyi kazi zao vizuri na lazima tujirekebishe kwa kusikiliza kero za wananchi." Makalla.

Vilevile, Mhe. Mkuu wa Mkoa ameutaka uongozi wa Wilaya na wataalamu wa ardhi wafike kwenye eneo lenye wadai 29 wa fidia waliopisha ujenzi wa kituo cha Mabasi cha wilaya hiyo kufanya tathmini na kamati ya fedha ijulishwe madai halali na yalipwe ili kuondoa kero hiyo inayowakabili wananchi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti