• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AAGIZA KUKOMESHWA KWA UVUVI HARAMU ZIWA VIKTORIA

Posted on: June 6th, 2023

RC MAKALLA AAGIZA KUKOMESHWA KWA UVUVI HARAMU ZIWA VIKTORIA


*Ataka kukomeshwa kwa uvu


*Ataka viongozi kudhibiti Uhamiaji haramu hususani kwenye visiwa*


*Aagiza kurudishwa kwa Mkandarasi aliyejenga barabara Nansio ambayo imebainika kuwa na kasoro*


*Amesisitiza nidhamu kazini pamoja na kushirikiana*


*Awataka Ukerewe kutunza miradi ya kimkakati*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, CPA Amos Makalla leo Juni 06, 2023 amefika Kisiwani Ukerewe akiwa katika Muendelezo wa ziara yake ya kikazi ya kujitambulisha akihakikisha anafika na kuzungumza na Viongozi na Watendaji katika Halmashauri zote za Mkoa huo.


Akizungumza wilayani Ukerewe, Mhe. Makalla ametoa wito kwa wanachi wa Ukerewe kuhakikisha wanafanya shughuli za uvuvi kwa mujibu wa sheria na sio kwa kuharibu mazalia ya samaki aidha ametoa wito kwa Kamati ya Usalama kusimamia hilo wakati wote ili kuimarisha uchumi wa jamii kupitia shughuli za uvuvi.

"Nafahamu ya kwamba Uvuvi ndio shughuli yetu kuu hapa lakini nimekuja kuwakumbusha kuvua kwa kuzingatia sheri tusitumie mabomu, nyavu haramu na aina yoyote ya Uvuvi haramu ili samaki waendelee kuzaliana kwani huo ndio uchumi wetu hivyo tukiharibu tutaharib uchumi wetu." Mhe. Makalla.

Aidha, ameiagiza idara ya Uhamiaji kushirikiana na wananchi hususani kwenye visiwa kuhakikisha hakuna Wahamiaji haramu kwani wilaya hiyo imetawanyika sana kijiografia kwa kuzingatia imezungukwa na visiwa 38 vidogo vidogo vikiwemo 15 vyenye makazi ya kudumu.

Vilevile, amemuagiza Mkuu wa Wilaya kwa kushirikiana na Meneja wa TARURA kuhakikisha mkandarasi aliyejenga barabara ya Mjini yenye urefu wa zaidi ya KM 1 kuhakikisha anaifanyia marekebisho kwenye kasoro zilizobainika ili wananchi wapate mradi wenye kiwango kinachokubalika na thamani ya fedha.

"Mhe. Mkuu wa Wilaya shirikiana na wenzako mrudisheni Mkandarasi aliyejenga barabara ya kiwango cha lami hapa mjini ambayo ina kasoro nyingi na kusababisha manung'uniko kwa wanamchi ili aje aifanyie marekebisho kuondoa kasoro hizo," amesisitiza.

Aidha, Mhe. Makalla amesisitiza kufuatwa kwa taratibu za fedha kwa kukusanya na kuwasilishwa benki kabla ya kuzitumia na akawataka watumishi kushirikiana na Mkaguzi wa ndani wa Halmashauri kujibu hoja za Ukaguzi kwa wakati ili kuifanya Halmashauri hiyo kuenenda kisheria.

Aidha, amesisitiza uadilifu kwa watumishi wa umma katika kuwahudumia wananchi na akatoa wito kwa viongozi kushirikiana na watendahi katika kusimamia miradi ya Maendeleo ili kujenga imani kwa wananchi dhidi ya Serikali yao inayoongozw na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mhe. Hassan Bomboko, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe amesema Wilaya hiyo iliyozungukwa na visiwa 38 vidogo vidogo ambapo 15 vina makaazi ya kudumu watu wake wana amani na wanaendelea na shughuli za kujitafutia ridhiki hususani kwa shughuli za uvuvi kwa amani.

Amesema Serikali kuu imekua ikiwajali sana kwani wamepokea zaidi ya Bilioni 12 ndani ya mwaka huu wa fedha kwa ajili ya kutekeleza Miradi mbalimbali katika Sekta za Nishati, Afya, Elimu, Miundombinu na Maji na kwenye hilo amemshukuru Mhe. Rais Samia kwa niaba ya wananchi wa kisiwa hicho.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti