• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AAGIZA UANDALIWE MPANGO MKAKATI WA KUKUZA SEKTA YA UTALII MKOA WA MWANZA

Posted on: November 30th, 2023

RC MAKALLA AAGIZA UANDALIWE MPANGO MKAKATI WA KUKUZA SEKTA  YA UTALII MKOA WA MWANZA.


*Amuagiza Katibu tawala Mkoa kuandaa kikosi kazi cha kuandaa mpango huo ukihusisha  wadau wa utalii


*Awataka kutumia miundombinu inayojengwa kuboresha utalii Mkoani humo*


*Abainisha kuwa mwezi Disemba mkataba wa Ujenzi wa Jengo la abiria uwanja wa Ndege Mwanza utasainiwa*


*Asema Mwanza ina mazingira mazuri ya Utalii wa Ziwa na ipo jirani na Hifadhi za Taifa kama Serengeti*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. CPA Amos Makalla amewataka wadau wa utalii Mkoani humo kutumia fursa ya uwepo wa mazingira rafiki ya ukanda wa ziwa, ujirani na hifadhi za Taifa na uwepo wa vivutio vya utalii kuboresha sekta hiyo kwa kuwekeza kwenye utalii kwa manufaa ya Taifa.


CPA Makalla amesema hayo mapema leo Novemba 30, 2023 kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakati wa kikao kazi na wadau wa utalii kilichokutuna mahsusi ili kujadili na kuweka mpango mkakati wa kuboresha sekta hiyo kwa kutumia mazingira rafiki kwenye ukanda huo uliobarikiwa.

Katika kuhakikisha suala hilo Mkuu wa Mkoa amemuagiza Katibu Tawala Mkoa kuunda kikosi kazi cha kuandaa mpango mkakati huo kikihusisha wataalam kutoka makundi mbalimbali ili kutoka na andiko linalojibu kila swali linalohusu namna gani sekta ya utalii mkoani humo itaboreshwa kwa manufaa ya wana Mwanza na Taifa kwa ujumla.


Amesema uwepo wa ziwa la kihistoria la Victoria, kufikika kwake kwa urahisi na hifadhi za Taifa kama Saanane, Burigi Chato, Rubondo, Rumanyika-Kagera na Serengeti pamoja na uwepo wa vivutio vya kitalii vya kihistoria kama Jiwe linalocheza lililopo Kisiwani Ukerewe, Jengo la Kijerumani la Gunsert na Bujora kunapaswa kusaidia kukuza sekta hiyo.

"Kwa takwimu zilizopo za idadi ya watu kuwa ni Mkoa wa pili, uwepo wa mifugo mingi, uvuvi, kilimo na uwanja wa ndege wa Mwanza ambao unaboreshwa ni ishara tosha kuwa wadau wakijipanga na kuchangamkia fursa zilizopo uchangiaji wa pato la Taifa utapanda na Mwanza itaongoza", amesisitiza.


Katika kuboresha utalii, Makalla amebainisha kuwa Serikali inaendelea kuboresha miundombinu kama ujenzi wa daraja kubwa la Kigongo-Busisi, Meli ya MV Mwanza pamoja na Bandari, Reli ya kisasa na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza pamoja na ujenzi wa jengo la abiria la kisasa ambapo mwezi Disemba mkataba wa ujenzi utasainiwa.


Halikadhalika, Makalla amewataka wataalam hususani kwenye Halmashauri kuweka nia ya kuboresha utalii, kuanisha vivutio vilivyopo na miundombinu inayotakiwa kama mahoteli yenye hadhi na kujipanga na mikakati ya kutenga maeneo yenye hadhi kuendana na utalii ili kujihakikishia kukuza sekta hiyo na kumuunga mkono Rais Samia ambaye amejipambanua kuitegemea sekta hiyo.


"Ndugu viongozi ni lazima tuthubutu kushawishi watu wenye mahoteli na kampuni za kusafirisha watalii, sekta binafsi lazima ihamasishwe, vyuo vikuu na vya kati lazima vichangie kwenye kuwajengea uwezo rasilimali watu na kuhakikisha wanachangia ukuaji wa sekta ya utalii." Mkuu wa Mkoa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti