• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AAGIZA UONGOZI JIJI LA MWANZA UREJESHAJI WAFANYABIASHARA SOKO KUU MWANZA UWE WA WAZI

Posted on: January 19th, 2024

RC MAKALLA AAGIZA UONGOZI JIJI LA MWANZA UREJESHAJI  WAFANYABIASHARA SOKO KUU MWANZA UWE WA WAZI


*Ataka Utaratibu wa kurejesha kuanza na wafanyabiashara walioondolewa awali*


*Asema hakuna Kizimba kulichotolewa kwa mfanyabiashara hadi sasa*


*Asema Mkandarasi atalipwa fedha baki wiki ijayo*


*Amshukuru Rais Samia kutoa fedha za Ujenzi wa Soko hilo*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewaagiza Halmashauri ya Jiji la Mwanza kuhakikisha Ugawaji wa Vizimba kwenye Soko Kuu la Mjini Kati mara litakapokamilika unakua wa Uwazi na wenye ushirikishaji wa Makundi ya Wafanyabiashara wenyewe.


Makalla ametoa agizo hilo leo tarehe 19 Januari 2024 wakati alipofika kwenye Soko hilo kukagua Maendeleo ya Ujenzi wake unaogharimu zaidi ya Bilioni 25 na kubaini kuwa wapo kwenye hatua za Ukamilishaji kwani wamefikia asilimia 93 ya ujenzi.

"Hili ndilo soko haswa lenye hadhi ya Jiji na Mkoa wa Mwanza, tunamshukuru sana Mhe. Rais kwa kutoa fedha za Ujenzi wa Soko lenye uwezo wa kubeba wafanyabiashara zaidi ya 1400 tofauti na 400 walioondolewa siku za nyuma kwenye soko hilo." Makalla.

Makalla amewatoa hofu wananchi wanaodhani kwamba tayari vizimba vimeanza kugawiwa kwenye eneo hilo na akatoa tamko kuwa hakuna hata kizimba kimoja ambacho kimetolewa kwa mfanyabiashara na kwamba watapewa kipaumbele walioondolewa kwenye soko la zamani.

Vilevile, amebainisha kuwa wiki ijayo Mkandarasi atalipwa Bilioni 1.3 zilizobaki kwenye mradi huo hivyo anapaswa kuongeza spidi ya ujenzi ili mwezi Machi amalize ujenzi na kukabidhi Soko hilo ili wafanyabiashara warejeshwe na wengine wanufaike nalo.

Meya wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza Mhe. Sima Costantine amebainisha kuwa kupitia Bilioni 2 zilizotengwa kwa ajili ya Miundombinu zitasaidia kuweka sawa kwenye uhimarishaji wa barabara ya kuingia kwenye Soko hilo ili wafanyabiashara wapate urahisi kwenye shughuli zao.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti