• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AMEWATAKA WANANCHI KULINDA VIFAA VYA MRADI WA SGR

Posted on: June 2nd, 2023

RC MAKALLA AMEWATAKA WANANCHI KULINDA VIFAA VYA MRADI WA SGR


*Aomba ushirikiano katika kuwaletea maendeleo wananchi*


*Aipongeza Kwimba kwa mafanikio, aiangazia michezo*


*Asisitiza kudumishwa kwa Usalama kwa wananchi*


*Awataka viongozi kutoa elimu dhidi ya madhara ya imani za Kishirikina*


*Ana imani kubwa na nidhamu kazini kama dira ya Maendeleo*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amempongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutekeleza miradi ya kimkakati nchini hususani mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) na amewataka wananchi kulinda Miundombinu hiyo kizalendo ili ufikie adhama ya kukuza uchumi wa nchi.

Akizungumza na viongozi, watendaji na makundi mbalimbali leo tarehe 02 Juni, 2023 kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba Mhe. Makala amesema uchumi wa nchi utakua zaidi kupitia Miradi ya kimkakati hivyo ni lazima wananchi wawe wazalendo kuilinda kusiwe na upotevu wa vifaa wakati wa utekelezaji.

"Tukiruhusu wizi wa vifaa na mafuta kwenye miradi yetu tunajiibia wenyewe na tunajichelewesha kupata maendeleo, nawaomba wana Kwimba tulinde mradi wa SGR na tuhakikishe vifaa kwenye kambi ya Ujenzi iliyopo hapa haviibiwi kwani mradi huo ukikamilika tutasafirisha Pamba kwa haraka sana na tutakuwa kiuchumi." CPA Makalla.

Aidha, ametumia wasaa huo kuomba ushirikiano kwa viongozi na watumishi wote huku wakitanguliza nidhamu mahala pa kazi ili kwa pamoja waweze kumsaidia Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kuwaletea maendeleo wananchi katika kila sekta hususani za kilimo, uvuvi, uchimbaji madini na biashara.


Vilevile, ameipongeza wilaya hiyo kwa mafanikio na maendeleo makubwa waliyofikia tofauti na siku za nyuma na kwamba amewataka kuendelea kudumisha amani ili kuhakikisha wananchi wanakuwa na uhuru wa kufanya kazi za maendeleo na kuacha tabia za kufanya ramli chonganishi.

"Inashangaza kuona Chuo cha michezo nchini kipo hapa Kwimba kinaitwa Malya ila Mkoa huu hauna timu kwenye ligi kuu, ni lazima tufanye mageuzi kwenye michezo ili chuo hiki kitunufaishe kwanza sisi wenyewe na turudishe furaha kwa wananchi wa Mwanza", Mhe. Makalla akizungumzia Michezo.


Naye, Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija amesema wananchi wa wilaya hiyo wanaendelea na uzalishaji ambapo kwa sasa wapo kwenye mavuno ya Pamba, Mahindi na Mpunga lakini vilevile wanalima choroko kwa amani kutokana na kazi nzuri inayofanya na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Sungusungu.

"Tunaendelea kufanya mikutano kwa wananchi tukiwakumbusha kutunza chakula kwa ajili ya siku za baadae kwani kwa kuzingatia historia ya msimu uliopita hawakufanikisha mavuno mengi hivyo ni lazima kuweka akiba na tunahakikisha pembejeo za kilimo zinawafikia wakulima wetu kwa wakati," amesema Mhe. Ludigija

Ameongeza kuwa kwa mwaka wa fedha uliopita Halmashauri hiyo ilitengewa Bilioni 20 kutekeleza miradi ya maendeleo na  hadi sasa wamepokea zaidi ya fedha hizo lakini vilevile Halmashauri hiyo inayotegemea kukusanya kupitia kilimo wameshakusanya Bilioni 3.2 ambapo ni sawa na 97% ya makadirio.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti