• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AMTAMBULISHA RASMI KOCHA MKUU WA PAMBA JIJI FC, MBWANA MAKATTA

Posted on: July 25th, 2023

RC MAKALLA AMTAMBULISHA RASMI KOCHA MKUU WA PAMBA JIJI FC, MBWANA MAKATTA


*Atambulisha jina jipya la timu kuwa ni Pamba Jiji Football Club*


*Asema timu imempata kocha mwenye viwango na uzoefu wa mechi za Ligi kuu*


*Awaomba wana Mwanza kuunganisha nguvu zao ili timu ipande Ligi kuu msimu ujao*


Hatimaye timu ya soka ya Pamba Jiji FC ya Mkoani Mwanza inayoshiriki  Ligi ya Championship imempata kocha Mkuu mpya Mbwana Makatta akisaidiana na msaidizi wake, Renatus Shija aliyeingia kandarasi ya mwaka mmoja ya kuinoa timu hiyo maarufu kama TP LINDANDA.

Akimtambulisha leo mbele ya vyombo vya Habari kwenye ukumbi mkubwa wa Ofisi yake, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Amos Makalla ambaye ni mlezi wa timu hiyo amebainisha baada ya kufanya mchakato wa kina hatimaye wamempata mtaalamu huyo wa ufundi wa uhakika.

"Namtambulisha kwenu kocha mpya Mbwana Makatta, hapa nawahakikishieni hatukubahatisha kumpata,namfahanu vyema uwezo wake na nina imani tutafika malengo yetu ya kucheza Ligi kuu msimu ujao,"CPA Makalla.

Mkuu huyo wa Mkoa ambaye ni mkereketwa wa michezo amesema baada ya kuimarisha dawati hilo la ufundi, kinachofuata sasa ni maandalizi ya timu kuingia kambini Agosti Mosi 2023 huku mtaalamu huyo wa ufundi akiendelea kuipitia ripoti ya mtangulizi wake na yeye kutoa mapendekezo yake baada ya kuwaona wachezaji uwezo wao.

"Kocha nikuondoe shaka tuna kasumba baadhi yetu kuwa na orodha ya nani umpange nani umwache katika mchezo husika,hilo la kuingiliwa hapa hutaliona na badala yake uamuzi wa mwisho utabaki kwako hata kama mimi nina mahaba na mchezaji fulani hilo lisikukwaze",amesisitiza mlezi wa timu hiyo.

"Nashukuru kwa wamiliki wa timu hii ambao ni Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa kuniamini kushika nafasi hii,nina wahaidi sitowaangusha katika kufikia malengo ya kucheza Ligi kuu msimu ujao,"Mbwana Makatta,Kocha Pamba Jiji FC

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza ambao ndiyo wamiliki wa timu hiyo,Aaron Karugumjuli amebainisha kazi iliyo mbele yao ni kumpa ushirikiano kocha huyo ili kukata kiu ya wana Mwanza ya kuona timu yao ikishiriki Ligi kuu.

"Kocha Mbwana ni mzoefu na amefundisha miaka ya nyuma timu ya hapa Mwanza ya Alliance,siyo mgeni na anarudi nyumbani kwa mara nyingine kuja kuinoa Pamba Jiji FC,karibu sana na tutakupa ushirikiano wa kutosha," Mhe.Sima Constantine Sima,Meya wa Jiji la Mwanza.

Timu ya Pamba Jiji FC mara ya mwisho kucheza Ligi kuu ni mwaka 1999 iliposhuka daraja.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti