• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA ARIDHISHWA NA MANDHARI YA SOKO KUU LA MJINI KATI LINALOENDELEA KUJENGWA

Posted on: July 17th, 2023

RC MAKALLA ARIDHISHWA NA MANDHARI YA SOKO KUU LA MJINI KATI LINALOENDELEA KUJENGWA.


*Amuhimiza Mkandarasi kulikamilisha kwa wakati.


*Autaka uongozi wa Jiji kupunguza minada ili mzunguko wa kibiashara uwe mzuri kwa wafanyabiashara wa soko kuu.


*Asisitiza pia kwa wenye ulemavu kupewa kipaumbele wa vizimba soko kuu


Mkandarasi Mohammed Buiders anayejenga Soko Kuu la mjini kati ametakiwa kufanya kazi kwa kasi zaidi  kwa lengo la wafanyabiashara waanze kufanya shughuli zao kwenye mazingira ya kisasa zaidi.

Akizungumza leo na uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza pamoja na Mkandarasi wa soko hilo mara baada ya kufanya ziara ya ukaguzi,Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,Mhe.CPA Amos Makalla amesema ameridhika na mandhari ya soko hilo jambo la msingi sasa ni wananchi kuharakishiwa huduma.


"Hili ni soko la mfano linalokwenda na hadhi ya Jiji letu la Mwanza,nimejionea maeneo yote ni ya kisasa na ukubwa wa huduma za aina mbalimbali",CPA Makalla.

Amesema amesikia taarifa ya ujenzi huo utakamilika Septemba mwaka huu baada ya kuomba kuongezewe muda,na ana matumaini kazi hiyo itakamilika kwa wakati na ataendelea kufuatilia.

Aidha ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Jiji kuona namna ya kupunguza minada inayofanyika maeneo mengi Jijini humo ili kuwepo na mzunguko mzuri wa kibiashara kwa wafanyabiashara kwenye soko hilo litakapoanza.


"Nilifanya mazungumzo na nduge zetu wenye ulemavu nawakumbusha uongozi wapewe kipaumbele kwa kutengewa maeneo yao kwenye soko hili kusiwepo na aina yoyote ya ubaguzi",amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa

Awali akimkaribisha Mkuu huyo wa Mkoa,Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana,Mhe.Amina Makilagi amesema mara baada ya kukamilika kwa soko hilo litapunguza bugudha wanayopata wafanyabiashara ndogo ndogo ambao bado wapo wengi mitaani.


"Soko hilo litachukua jumla ya wafanya biashara 1,400 watapata nafasi kwenye maduka 472 ya wafanyabiashara wadogo,wa kati na wakubwa",Mhe. Amina Makilagi,Mkuu wa Wilaya Nyamagana.


Kwa upande wake Mbunge wa Nyamagana Mhe.Stanslaus Mabula amebainisha wanamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa kuuwezesha Mkoa wa Mwanza miradi mbalimbali ya kuwaletea maendeleo wananchi.

Zaidi ya Shs Bilioni 23 zimegharimu ujenzi wa soko hilo ambalo hadi sasa limefikia asilimia 90.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti