• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA ATOA MAAGIZO KUKITHIRI KWA MIGOGORO YA ARDHI JIJI LA MWANZA.

Posted on: October 13th, 2023

RC MAKALLA ATOA MAAGIZO KUKITHIRI KWA MIGOGORO YA ARDHI JIJI LA MWANZA


*Awataka watumishi wa Idara ya Ardhi kubadilika na kushughulikia kero za wananchi mapema*


*Ameliagiza Jiji la Mwanza kuhakiki na kulipa fidia kwa maeneo yaliyotwaliwa na Serikali*


*Aagiza Halmashauri ya Jiji kuzingatia mpango kabambe wa Ujenzi*


*Ayataka makampuni ya Ulinzi kuzingatia sheria na kanuni kwa wanaowaajiri*


*Awaagiza watendaji wa Serikali kuwa wepesi kusikiliza wananchi wakati wote na kuwasaidia*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla ameanza ziara ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi pamoja na kukagua miradi ya Maendeleo kwenye halmashauri zote za mkoa huo ambapo leo Oktoba 12, 2023 amewasikiliza wananchi wa Nyamagana kwa zaidi ya saa nane (8).

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Makalla amewataka watumishi wa Idara ya Ardhi-Jiji la Mwanza kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake watatue changamoto za wananchi ili kuepusha migogoro.

Amesema, kukithiri kwa kero za ardhi katika mkutano wake ni ishara kwamba idara hiyo haifanyi kazi zake ipasavyo na kwamba jambo hilo limepelekea jamii kukosa Imani nao kwani kumekua na urasimu usio na lazima ambao umekua ukikwamisha kusonga mbele kwa sekta hiyo.

"Jiji la Mwanza lina migogoro mingi ambayo imechangiwa na watendaji wa idara hiyo kutotatua kero za wananchi na badala yake kunakua na urasimu kwenye kushughulikia, napenda niwaambie kwamba kwa sasa mambo hayo hayana nafasi nataka muende na falsafa ya kushughulikia kero." CPA Makalla.


Vilevile, Mhe. Makalla ameagiza kuhakikiwa kwa maeneo yaliyotwawaliwa na Serikali kama maeneo ya shule pamoja na vituo vya kutolea huduma za afya ili yalipwe fidia na kuwe na mpango wa kuhakiki na kulipa mara moja na sio kulimbikiza usuluhishi hadi kupelekea migogoro.


Aidha, amewaagiza jiji hilo kuzingatia mpango kabambe wa Ujenzi ili kuepusha athari za ujenzi holela na uchafuzi wa mji kwa kuruhusu mabadiriko yasiyostahili ambayo hupelekea ujenzi holela na kuharibu mandhari ya jiji hilo.


CPA Makalla ametumia pia wasaa huo kuwataka wamiliki wa makampuni ya ulinzi mkoani humo kuhakikisha wanazingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi ili kuwa na ajira zinazozingatia sheria na kuepusha migogoro.


"Msiogope hii ni fursa yenu ya kuonana moja kwa moja na Mkuu wenu wa Mkoa, njoo eleza kero yako maana nimekuja kusikiliza na kutatua kero zenu na kuwashauri pia namna ya kuepuka migogoro, nafasi hiyo ipo njooni." CPA Makalla akiwakaribisha wananchi.

Awali akimkaribisha Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi amemshukuru kwa kusikiliza wananchi wa wilaya hiyo na kutatua kero zao ikiwa ni wilaya ya kwanza ya usikilizaji wa kero na akamuahidi kuwa wataendelea kusikiliza wananchi na kuwaondolea adha.


Ziara ya usikilizaji kero za wananchi imekuja kufuatia uzinduzi rasmi wa ngazi ya Mkoa uliofanywa tarehe 18 Septemba, 2023 ambapo alisikiliza kero 78 na Mhe. Mkuu wa Mkoa akaahidi kufanya ziara kabambe ya kusikiliza wananchi kwenye wilaya zote ili kuwatatulia kero zao.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti