• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA ATOA MAAGIZO KWA WATAALAM WA KILIMO KUONGEZA TIJA ZAO LA PAMBA NA UTOSHELEVU WA CHAKULA MWANZA

Posted on: December 20th, 2023

RC MAKALLA ATOA MAAGIZO KWA WATAALAM WA KILIMO KUONGEZA TIJA ZAO LA PAMBA NA UTOSHELEVU WA CHAKULA MWANZA


*Ataka mkakati wa kuhakikisha Tija inaongezeka kwenye Mazao hususani Pamba*


*Aagiza Maafisa Ugani kutimiza Majukumu yao ya Msingi ya kuelimisha wakulima*


*Awaagiza Wakurugenzi kuwawezesha Maafisa Ugani nao kuwajibika kuwafikia wakulima*


*Awataka Mawakala kusogeza maduka ya Mbolea kwa Wakulima*


*Aagiza wataalam wa kilimo kujengewa uwezo ili kupeana uelewa*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka wataalam wa Kilimo kuhakikisha wanaweka

Mikakati ya kuongeza Tija kwenye uzalishaji wa zao la Pamba na Mazao ya Chakula ili Mkoa uwe na utoshelevu wa chakula na kuinua uchumi.


CPA Makalla ametoa wito huo mapema leo Disemba 20, 2023 kwenye Mkutano wake na Wadau wa Kilimo ikiwa ni muendelezo wa Vikao kazi vya kisekta vya kujadili namna ya kuongeza tija ambapo kupitia Kikao hicho ameagiza Uzalishaji wa Kisasa wa Mazao ya Chakula na biashara hususani pamba.

Mkuu huyo wa Mkoa ameongeza kuwa mradi wa vijana kwenye kilimo kupitia programu ya Kesho Bora Zaidi unaoratibiwa na Wzara ya Kilimo ni lazima uenziwe kwa kujitambulisha kuwa zao lipi ni la biashara na linategemewa kuwainua kwenye uchumi wananchi wengi na zao gani ni la pili kwa uzalishaji Mwanza.

"Mwanza hatupaswi kwenda shaghalabagala ni lazima tutimize wajibu wetu ili ufike wakati tujitambulishe kwa kuwa na zao letu kuu la biashara, hivyo Maafisa ugani na wataalam kutoka Mkoani ni lazima tuwe na Mkakati wa kuinua kilimo kwa wananchi wetu." Amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

Amesema zao la pamba limekua likishuka kwa uzalishaji mwaka hadi mwaka pamoja na kuwa na ardhi ya kutosha na mifugo haifanyi vizuri hilo ni jambo baya kwa maendeleo ya Taifa na kwamba tumefika hapo kutokana na wataalam katika kata kutokua na mkakati wa kusaidia wakulima kwa kuwafundisha kanuni bora za kilimo pamoja na mazao mengine ya chakula.


"Tunataka Ekari Moja ya shamba izalishe kilo elfu 1 ya Pamba na sio kilo 200 wanazopata wakulima hivi sasa kwani hata Mhe. Rais katika kuhakikisha zao hili linaimarika amehakikisha wataalam wa kilimo wana usafiri wa kuwafikisha moja kwa moja shambani, sasa Wakurugenzi ni lazima muwajibike kwa kuwapatia mafuta." Mhe. Makalla.


Aidha, Makalla amesema taasisi kama TOSC, Taasisi ya Utafiti TARI Ukiriguru, Taasisi inayosimia Ubora wa Udongo, Chuo cha Kilimo cha Ukiriguru na Shamba la Mifugo Mabuki ambazo zipo Mwanza ni lazima ziwajibike ilivyokusudiwa na kuonesha uwepo wake wa kuwasaidia wakulima kuongeza tija kwenye mazao.

"Udongo na Mbegu bora zinaweza kutupa matokeo mazuri sana kwenye kilimo na katika hilo Mhe. Rais ameonesha kwa mfano kwenye ruzuku na kuimarisha taasisi mahsusi inayoshughulikia Mbegu ili kuwe na uzalishaji mzuri wa mazao na uwepo wa Maduka ya mbolea jirani na wakulima." Mkuu wa Mkoa.


Afisa Kilimo kutoka Ofisi ya Mkoa Innocent Keya amebainisha kuwa Mahitaji ya Usambazaji wa Pembejeo za Pamba 2023/24 Mkoa umekadiria kutumia tani 1.972 za mbegu za Pamba na Chupa 901,036 za viuadudu na kwamba hadi kufikia Disemba 04, 2023 tani 1.742 za Mbegu zimesambazwa Halmashauri zinazolima Pamba na tani 1, 671 zimegawiwa kwa wakulima.


"Kufikia Juni 2023 wakulima 36, 992 wamesajiriwa katika Mfumo na hadi kufikia Disemba 18, 2023 wakulima 58, 596 walikua wamesajiriwa na 4, 362 walikua wamenunua mifuko 37, 282 (Tani 1.864) ya Mbolea." Amesema Keya wakati akizungumzia Changamoto za Kilimo Mwanza ikiwemo upungufu wa Maafisa Ugani kwa 260 kati ya 755 wanaohitajika.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti