• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA ATOA MAAGIZO KWA WAVAMIZI WA SHAMBA LA MIFUGO MABUKI-MISUNGWI

Posted on: January 18th, 2024

RC MAKALLA ATOA MAAGIZO KWA WAVAMIZI WA SHAMBA LA MIFUGO MABUKI-MISUNGWI


*Aagiza uongozi Mabuki, jeshi la polisi wilayani humo kufanya ukaguzi kubaini wavamizi wote*


*Asema Rais Samia anaziishi fikra za Mwl Nyerere kwa kutoa Ng'ombe jike (Mitamba) 500*


*Awapongeza wanafunzi  wa BBT kwa mafunzo mazuri ya ufugaji wa kisasa*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amelitaka jeshi la polisi wilayani Misungwi kwa kushirikiana na uongozi wa shamba la mifugo la Mabuki kuweka mipaka ya eneo lote la hekari elfu 25 na kuwabaini wavamizi ili mkuu wa wilaya hiyo awaondoe mara moja kwa ustawi wa shamba hilo.

Ametoa agizo hilo leo tarehe 18 Januari, 2024 wilayani Misungwi baada ya kupokea changamoto ya wananchi wakiwa na mifugo mingi kuvamia shamba hilo na kuathiri shughuli za utafiti, uzalishaji na Utoaji wa mafunzo kwa wafugaji jambo linalofanywa na wananchi kutoka kwenye kata nne zinazozunguka shamba hilo.

"Malengo ya kuanzishwa kwa taasisi hii na kuenzi fedha nyingi anazozileta Mhe. Rais Samia kwenye shamba hilo lazima ziwe na tija maana wavamizi ndio wanaotaka taasisi hii ife, vijana wa mradi wa BBT LIFE wasifanikiwe, mifugo yetu ife kwa magonjwa na hatutakubali kufika huko." CPA Makalla.


Aidha, amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa ng'ombe majike 500 (Mitamba) kwenye shamba hilo ambao wamesaidia kuendeleza uzalishaji na kutolea mafunzo kwa wafugaji ya namna bora ya kuzalisha nyama na maziwa bora kupitia mafunzo ya muda mfupi na mrefu yatolewayo shambani hapo.

Aidha, awapongeza wanafunzi walio kwenye shamba hilo chini ya mradi wa Jenga Kesho Bora (BBT) kwa mafunzo mazuri waliyoyapata na akabainisha kuwa uvumilivu wao utawasaidia kujiajiri kwa kufanya shughuli za uzalishaji kupitia ufugaji wa kisasa waliojifunza.


Mhe. Paul Chacha, mkuu wa wilaya ya Misungwi ametoa onyo kwa wafugaji wanaoingiza mifugo kwenye shamba hilo kuacha mara moja ili kuhakikisha utafiti, uzalishaji na mafunzo yanafanikiwa kwa mujibu wa sheria za uanzishwaji wa shmaba hilo la mifugo.

Meneja wa Shamba hilo Leni Mwala ametumia wasaa huo kumshukuru Rais Samia kwa kuendeleza shamba hilo lililoanzishwa mwaka 1967 lenye hekari elfu 25 kwa kuwaletea ng'ombe jike 500 (Mitamba) mwaka 2022/23 ambao wamesaidia kuendeleza wafugaji na kujifunzia.

"Serikali ya awamu ya Sita imetushangaza kwa furaha maana inatimiza maono ya Baba wa Taifa letu Hayati Rais Nyerere kwa kutuletea Mitamba 500 jike kwa ajili ya kuwakuza na kutumika kuendeleza kwenye utafiti kwa manufaa ya jamii ya wana Mwanza." Mwala.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti