• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AUKABIDHI RASMI MWENGE WA UHURU SIMIYU,MIRADI YENYE KASORO AHAIDI KUIFANYIA KAZI HARAKA

Posted on: July 21st, 2023

RC MAKALLA AUKABIDHI RASMI MWENGE WA UHURU SIMIYU,MIRADI YENYE KASORO AHAIDI KUIFANYIA KAZI HARAKA


*Awapongeza wakimbiza Mwenge Kitaifa kwa ukakamavu na uwezo wa kukagua miradi


*Ajivunia ubora wa miradi yenye tija kwa wananchi iliyozinduliwa na Mwenge wa Kitaifa


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe CPA Amos Makalla leo ameukabidhi rasmi Mwenge wa Uhuru kwa Mkoa wa Simiyu na kujivunia miradi yote iliyozinduliwa na Mwenge huo yenye thamani ya Shs bilioni 21 itakuwa na tija kwa wananchi.

Akimkabidhi Mwenge huo kwenye viwanja vya shule ya msingi Kiloleli Wilayani Busega, kwa mwenzake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Dkt.Yahaya Nawanda,CPA Makalla amebainisha miradi michache iliyobainika na kasoro atahakikisha inafanyiwa kazi na kumpa taarifa kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Abdalla Shaib Kaim kabla ya Julai 31,2023

"Ndugu Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa,miradi ambayo imeonesha utata nakuahidi kutumia vyombo husika kama Takukuru ili kubaini tatizo na hatua za kisheria kuchukuliwa,"amesisitiza Mhe.Makalla.

Ameongeza kuwa Mwenge wa Uhuru umekimbizwa kwenye Wilaya zote 7 zenye jumla ya Halmashauri 8 kwa utulivu na usalama na wanajivunia miradi isiyopungua 50 imeonesha kuwa kwenye ubora na tija kwa wananchi wa Mwanza.

"Asanteni sana ndugu zangu wa Mwanza kwa ukarimu na mapokezi mazuri tangu tulipoingia Mkoani hapa Julai 13,2023,rai yangu kwa viongozi tuendelee kuchapa kazi na kuisimamia vizuri miradi yote inayotekelezwa Mkoani hapa yenye malengo ya kumletea maendeleo mwananchi,tuwe makini kubaini changamoto na kuzipatia ufumbuzi haraka na siyo hadi viongozi wa Kitaifa waingilie kati," amesema Abdallah Shaib Kaim,Kiongozi wa Kitaifa mbio za Mwenge wa Uhuru.

Kauli mbiu ya mbio za Mwenge wa Uhuru inasema "Tunza Mazingira,Okoa vyanzo vya Maji kwa Ustawi wa viumbe hai kwa Ustawi wa Taifa".

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti