• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AWAPA KONGOLE NMB KWA KUWAUNGANISHA WATEJA KATIKA MFUMO RASMI WA KIFEDHA

Posted on: September 15th, 2023

RC MAKALLA AWAPA KONGOLE NMB KWA KUWAUNGANISHA WATEJA KATIKA MFUMO RASMI WA KIFEDHA


*Asema kuwajumuisha watanzania kwenye mfumo rasmi wa kifedha kunasaidia kuinua kipato*


*Aipongeza kwa kubuni bidhaa zinazolenga mahitaji ya kila kundi kwenye soko na kwa kutoa mikopo*


*Atoa wito kuandaa programu kwa watumishi wengine wa serikali*


*Atoa wito kwa walimu kuhifadhi pesa benki na kuachana na mikopo yenye masharti magumu*


CPA Amos Makalla ameipongeza benki ya NMB kwa kuwatunza walimu kwa masuluhisho mbalimbali ya kifedha na kuunga mkono juhudi za Serikali za kuwajumuisha watanzania katika mfumo rasmi wa kifedha ili kuinua vipato vyao na uchumi kwa ujumla.

Ametoa pongezi hizo leo tarehe 15 septemba, 2023 kwenye warsha ya siku ya walimu iliyoandaliwa na benki hiyo ambayo imezindua mpango wa kuwafikia walimu zaidi ya 9,000 kote nchini kwa kaulimbiu ya "Mwalimu Spesho- Umetufunza Tunakutunza."

 "Nimeambiwa kuwa madhumuni ya siku hii ni pamoja na kutambua mahusiano mazuri yaliyopo na kutoa fursa kwa walimu kutoa maoni na mapendekezo ya namna gani wanaweza kunufaika zaidi na huduma za benki hii, hakika jambo hili linatupa faraja sana  kwakweli naomba niwapongeze sana NMB." Mhe. Mkuu wa Mkoa.


"Jitihada hizi ni nzuri na zinaunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya Sita katika kuhakikisha watanzania wanajumuishwa katika mfumo rasmi wa kifedha ili kuinua vipato vyao na uchumi kwa ujumla, natoa rai kwa mabenki na taasisi zingine za kifedha kuunga mkono ili elimu hii iwafikie wengi hasa maeneo ya vijijini." Amesisitiza Makalla.


Makalla amesema uamuzi wa kuwakutanisha walimu ni wa kizalendo na unafaa kuigwa na kila taasisi kwani unaonesha kuwajali walimu na utakuza mahusiano mazuri kati ya pande hizo mbili za benki na sekta ya elimu hapa nchini.


Vilevile, ametumia wasaa huo kuwapongeza kwa kubuni bidhaa zinazolenga mahitaji ya kila kundi kwenye soko na kwa kutoa mikopo mingi kwa wafanyakazi wa Serikali kuu na za mitaa ambapo asilimia kubwa ya walimu wananufaika nayo kwa kukidhi mahitaji ya familia na hata maandalizi ya maisha baada ya kustaafu.

"Nawasihi kuendelea kuandaa programu nyingi si kwa walimu tu hata kwa watumishi wengine wa Serikali ili kuwapa fursa ya kuongeza ufahamu wa huduma na muendelee kubuni huduma nafuu zaidi ambazo mfanyakazi wa kawaida anaweza kuzimudu." CPA. Makalla.

Aikansia Muro, Mkuu wa Idara ya wateja binafsi amesema kwa kipindi cha miaka 8 mfululizo wanakutana na walimu kwenye siku maalumu na makongamano hayo yamekua yakiwapa fursa kama wateja kuelimishwa juu ya huduma na inatoa nafasi kwa benki hiyo kupokea maoni juu ya huduma zao na kwenda kuziboresha.


"Benki ya NMB tutaendelea kuwa na masuluhisho bora ili kuwaleta watanzania pamoja na katika huduma bora za kifedha nchini, na tutaendelea kubuni huduma bora zaidi kwa ajili ya makundi yote nchini hata wafanyabiashara wadogo na wakulima." Bi. Aikansia.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti