• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AWATAKA MADIWANI KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: June 3rd, 2023

RC MAKALLA AWATAKA MADIWANI KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO


*Ataka ajenda ya kuthibiti uhalifu iwe ya kudumu*


*Asisitiza nidhamu kazini pamoja na kushirikiana*


*Awataka Misungwi kuitunza miradi ya kimkakati*


*Awataka wazazi kupeleka watoto shule*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo Juni 03, 2023 amefika wilayani Misungwi akiwa katika muendelezo wa ziara yake ya kikazi ya kujitambulisha rasmi kufuatia kuhamishiwa kwake Mkoani humo mwishoni mwa mwezi Mei.


Akizungumza na viongozi, watendaji na makundi mbalimbali katika Ukumbi wa Halmashauri ya wilaya hiyo Mhe. Makalla amewataka waheshimiwa Madiwani kusimamia miradi ya Maendeleo kwa dhati ili fedha zinazowekezwa huko zioneshe tija kwa kukamilisha miradi yenye ubora na thamani halisi ya fedha.

"Nataka kuwakumbusha juu ya kusimamia kwa dhati miradi ya Maendeleo ili inapokamilika iwe na ubora ila nawapongeza sana kwa kupeleka fedha za miradi ya Maendeleo kwa aslimia 40 na kwenye hili natoa wito kwa waheshimiwa madiwani kutimiza wajibu wao kupitia kamati zao ni lazima wawe na ratiba ya kutembelea na kuikagua miradi." CPA Makalla.

Aidha, Mhe. Makalla ametoa rai kwa viongozi na watumishi wilayani humo kuhakikisha wanakuwa na nidhamu na kuwajibika ipasavyo na kufanya kazi kwa kushirikiana ili kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kuwa na lugha ya staha na kutoa matumaini kwa jamii.


"Misungwi inakwenda kuwa na kituo cha mizigo kupitia mradi wa reli ya kisasa (SGR) hivyo basi hapa ni sehemu ya kibiashara na mna bahati sana kwani Miradi mikubwa ya kimkakati inagusa wilaya yenu hivyo niwaombe muitunze miradi hii kusiwe na wizi wa vifaa." Mkuu wa Mkoa.

Akitoa taarifa ya Wilaya hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe. Paulo Chacha amesema wilaya hiyo yenye zaidi ya watu laki nne wananchi wake wamekuwa wakijishughulisha na shuguli mbalimbali za kujikwamua kiuchumi zikiwemo Kilimo na Uvuvi kwa zaidi ya asilimia 90 pamoja na biashara na uchimbaji wa Madini.


Aidha, amebainisha kuwa wananchi wa Wilaya hiyo wamenufaika na fidia ya zaidi ya Shilingi Bilioni 7 walizolipwa  kupisha maeneo yao kwa utekelezaji wa miradi ya Reli ya Kisasa (SGR) pamoja na Bandari kavu na wamekuwa wazalendo kuhakikisha uwekezaji wa aina yoyote haukwami.


"Katika kuhakikisha wananchi wa Misungwi wanakuwa na afya njema, afua mbalimbali zinatekelezwa ikiwemo utoaji wa Elimu ya Lishe kwenye shule za Msingi na Sekondari na Ugawaji wa dawa kama za floriki na utoaji wa chakula chenye lishe bora ili kuwakinga watoto na Utapiamlo na kwamba wananchi wanapata huduma ya Maji safi na salama kupitia mamlaka husika." Amefafanua.

Mhe. Chacha anajivunia hati Safi wanazopata mfululizo na amefafanua kuwa Halmashauri hiyo imekua ikikuwa kimakusanyo kila mwaka kutoka Bilioni 2 zilizokusanywa mwaka 2021/22 na Bilioni 3 zilizokusanywa kwenye mwaka 2022/23 na kwamba kwa mwaka 2023/24 wamekadiria kukusanya Bilioni 4.86 na tayari kuna mikakati madhubuti ya kufanikisha hilo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti