• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AWATAKA PAMBA JIJI FC KUJITUMA NA KUPATA MATOKEO MAZURI UWANJANI

Posted on: October 13th, 2023

RC MAKALLA AWATAKA PAMBA JIJI FC KUJITUMA NA KUPATA MATOKEO MAZURI UWANJANI


*Asema hafurahishwi na mwenendo wa sasa wachezaji kutokujituma na kupata matokeo yasiyoridhisha*


*Awataka kubadilika kuanzia mchezo wao ujao*


*Awahaidi changamoto zao kuzifanyia kazi*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka wachezaji wa Pamba Jiji FC kujitafakari haraka kabla ya mchezo wao ujao wa Ligi ya Championship  kutokana na matokeo yasiyoridhisha.

Mkuu huyo wa Mkoa ambaye ni mlezi wa timu hiyo amezungumza leo Oktoba 10, 2023 mara baada ya mazoezi yao kwenye uwanja wa Nyamagana, amebainisha  hali halisi ni wachezaji kutojituma uwanjani ndiyo maana timu imepata matokeo yasiyoridhisha na kushika nafasi ya saba na pointi 7.

"Nimezungumza na makocha kadhaa wa Ligi ya Championship wanasema wazi kabisa tumefanya usajili bora hadi dawati la ufundi lakini changamoto tuliyonayo ni kucheza chini ya kiwango na tusipo badilika haraka itatugharimu", CPA Makalla.

Ameongeza kuwa lengo ni timu kucheza Ligi kuu msimu ujao ndiyo maana imefanyiwa maandalizi mazuri ya kutoka kuchangiwa bakuli na sasa inamilikiwa na Halmashauri ya Jiji na endapo hakutakuwa na mabadiliko juhudi za haraka za kuongeza nguvu za wachezaji kutoka nchi jirani zitafanywa wakati wa dirisha dogo.

CPA Makalla akiwa ameambatana na baadhi ya wachezaji wa zamani wa Pamba FC akiwemo Fumo Felician naye alipata wasaa wa kuwatia shime kucheza kwa bidii kama walivyofanya wao miaka ya nyuma.

"Tambueni mnaichezea timu yenye jina kubwa hapa nchini,huu ni wakati wa kutupa matokeo mazuri kutokana na mazingira mliyonayo,sisi miaka ya nyuma maslahi hayakuwa makubwa zaidi ya kucheza kwa uzalendo na kuupambania Mkoa". Fumo Felician, mshambuliaji wa zamani,Pamba FC


"Mhe.Mkuu wa Mkoa tumekusikia ila changamoto inayotukabili ni timu nyingi kutupania kila tukicheza nazo, tunatambua matokeo haya hayawafurahishi mashabiki wa soka tunawaahidi kujirekebishia,"Jerry Tegete,Nahodha wa timu.

Pamba Jiji FC baada ya kucheza michezo 5 ikishinda miwili, imepoteza mmoja na kutoka sare, hata hivyo jumamosi hii itashuka uwanja wa nyumbani Nyamagana kupepetana na Green Warriors.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti