• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AWATAKA USHIRIKA KUTOA ELIMU KWA WAKULIMA JUU YA FAIDA ZA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI

Posted on: January 11th, 2024

RC MAKALLA AWATAKA USHIRIKA KUTOA ELIMU KWA WAKULIMA JUU YA FAIDA ZA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI


*Awataka vyama vya ushirika kutoa elimu ya faida za mfumo huo*


*Amesema mfumo huo unatoa uhakika wa soko la mazao*


*Aziagiza Halmashauri kukutana na wadau wilayani*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka Wadau wa ushirika kutoa elimu ya kutosha kwa wakulima juu ya faida za mauzo ya mazao kwa mfumo wa stakabadhi ghalani kwa maendeleo ya sekta hiyo.

Mkuu wa Mkoa ametoa maagizo hayo mapema leo Januari 11, 2024  wakati wa kikao cha wadau wa ushirika kilicholenga kujadili utekelezaji wa mfumo wa stakabadhi ghalani kwa mazao ya choroko na dengu 2023/24.

Amesema, wakulima wanataka kuona wanapata bei nzuri kwenye mazao kufuatia kuwekeza muda na nguvu kwenye kilimo kwa msimu mzima aidha kwa mikopo kutoka kwenye mabenki hivyo wanachohitaji ni kufahamishwa manufaa ya mfumo huo.

"Serikali inatambua mchango wa mfumo huu na umesaidia kuchochea wakulima kupata soko la uhakika lenye tija, mfumo huu umesaidia wakulima kwenye mazao kama kakao, korosho na ufuta na kwamba umekuza huduma za kifedha vijijini." Mkuu wa Mkoa.

Vilevile, amefafanua kuwa Mfumo wa stakabadhi ghalani una manufaa makubwa sana na umesaidia wakulima kutumia mzani halisi na kuongeza kipato kwa misimu miwili ya 2020 hadi 2022 na sasa Serikali imejipanga kuboresha zaidi huduma ili mkulima anufaike zaidi.

Robert Sunza kutoka Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini amesema wao kama wahamasishaji na wasimamizi wa maendeleo ya ushirika na kwenye mfumo huo unasaidia kupata ubora wa bidhaa, ushindani wa bei kutoka kwa wanunuzi na kupata takwimu za uhakika.

"Vilevile mfumo wa stakabadhi za ghala unasaidia kuongeza uzalishaji, mapato, miundombinu ya uhifadhi, usimamizi pamoja na kuimarika kwa biashara kutokana na kuongezeka kwa wanunuzi." Amefafanua ndugu Sunza.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti