• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AWATAKA WADAU MKOANI HUMO KUTOA MAONI YA KINA KWENYE DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050

Posted on: July 24th, 2023

RC MAKALLA AWATAKA WADAU MKOANI HUMO KUTOA MAONI YA KINA KWENYE DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050


*Azitaka Taasisi kuainisha Vipaumbele vya Bajeti na Maendeleo ya Jamii*


*Atoa wito kwa Sekta za Uvuvi, Kilimo cha Pamba na Uchimbaji wa Madini kushiriki kikamilifu*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka Wadau Mkoani humo kushiriki vema katika kutoa Maoni ya Kitaalamu katika kuhakikisha wanachangia vema kwenye upatikanaji wa Dira Bora ya Maendeleo 2050.

Ametoa wito huo leo tarehe 24 Julai 2023 wakati akifungua Warsha ya Uelimishaji Umma juu ya uandaaji wa Dira ya Taifa 2050 iliyowakutanisha Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala Wilaya, Wakurugenzi, Wakuu wa Seksheni na Vitengo na Wakuu wa Taasisi mbalimbali.

Makalla amesema, katika kupanga malengo ya muda mrefu kama Dira ya Maendeleo ni lazima kila taasisi iainishe Vipaumbele, Bajeti na Maendeleo ya Jamii hivyo ni lazima kuthamini fursa waliyoipata ya kuwa sehemu ya kuchangia maoni na kuitumia vema.

"Ni kikao chetu muhimu sana katika kuelekea maendeleo endelevu ya miaka ya mbele mathalani jeshi la Polisi lazima liweze kupanga linataka liwe la aina gani kwa mfano kwenye kupambana na wizi wa kimtandao." CPA Makalla.

Aidha, Mhe. Makalla amezitaka Sekta kuu za kiuchumi kama Uvuvi, Kilimo cha Pamba, Uchimbaji wa Madini kupanga vema kwenye vipaumbele mahususi vitakavyokuza sekta zao kiuchumi ili kusaidia wananchi walio wengi maana ndizo shughuli kuu za kiuchumi Mkoani humo.

"Taifa letu limekua na Dira ya Maendeleo ya kuishia 2025 na sasa Serikali ipo kwenye maandalizi ya dira kuelekea 2050 ambapo tumekutana makundi mbalimbali kwa kushirikiana na ngazi ya Taifa katika kuhakikisha kila kundi linahusika kwenye kutoa maoni." Amesema Katibu Tawala Mkoa, Balandya Elikana.

Bwana Omary Othman, Mjumbe wa Maandalizi ya Dira ya Maendeleo ya Taifa amesema wanahamasisha na kutoa elimu ili kupata ufahamu wa pamoja na kwamba wanategemea viongozi wa Mkoa husika watapeleka elimu hiyo hadi chini ili wananchi waweze kushiriki vema kutoa maoni wakati wa zoezi hilo utakapofika.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti