• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AWATAKA WADAU WA ELIMU MWANZA KUBORESHA ELIMU, KUAINISHA MIPAKA YA SHULE MAPEMA

Posted on: July 27th, 2023

RC MAKALLA AWATAKA WADAU WA ELIMU MWANZA KUBORESHA ELIMU, KUAINISHA MIPAKA YA SHULE MAPEMA


*Asema kipaumbele chake ni kuboresha elimu, kuongeza ufaulu*


*Wazazi waelimishwe kuhusu umuhimu wa kuchangia chakula kwa wanafunzi*


*Amshukuru Rais Samia kwa kuleta fedha nyingi kwenye miradi ya elimu*


*Wakuu wa Wilaya awataka kusimamia mikutano ya kuboresha elimu kwenye maeneo yao*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Amos Makalla amewataka wadau wa elimu Mkoani humo  kusimamia vyema

maendeleo ya elimu na kuepuka migogoro ya ardhi kwa kuainisha mipaka yao mapema kwa kuweka beacon.

Akizungumza leo na wadau wa elimu kutoka Wilaya zote za Mkoa huo kwenye ukumbi wa Shule ya Sekondari Loreto, Mkuu huyo wa Mkoa amesema uboreshwaji wa elimu utakuwa na mafanikio endapo kila mmoja atatimiza wajibu wake kwa weledi kuanzia ngazi ya Maafisa elimu kata.

"Leo tupo hapa yakiwa ni maelekezo yangu ya kutaka tukutane na tupeane mikakati kamambe ya namna ya kuboresha elimu Mkoani kwetu,bado zipo changamoto za hapa na pale ambazo tukienda kuzisimamia vyema tutafika katika malengo yetu",CPA Amos Makalla.

Amesema Serikali ya Rais Samia imeleta fedha nyingi kuboreha Sekta ya elimu Mkoani Mwanza ikiwemo shule ya wasichana Magu ya kidato cha tano na sita iliyogjarimu Shs bilioni 3,wajibu wa wadau hao ni kuhakikisha wanajituma ili kuleta matokeo chanya

Amewaagiza wadau hao kutoa nafasi ya kutosha ya kuwaelimisha wazazi na walezi wa kuona umuhimu wa kuchangia chakula shuleni hali ambayo italeta tija kwa wanafunzi ya kuwa na usikivu mzuri wa masomo na hatimaye kufanya vyema katika masomo yao.

"Hapa nawaomba tuelewane vizuri tutangulize busara katika kuwaelimisha wazazi,epukeni kutumia aina yoyote ya nguvu, vitisho au kumrudisha mtoto nyumbani,wakuu wa Wilaya muwe mstari wa mbele kusimamia mikutano hii ili kuwepo na upana mzuri wa uelewa katika jambo hili",amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Kuhusu suala la utoro shuleni,Makalla amewataka wakuu wa Shule kufanya ufuatiliaji kwani Serikali imesha weka mazingira mazuri ya watoto kusoma kwa kuondoa malipo ya ada.

Ameongeza kuwa wapo baadhi ya wazazi  wanaowatumikisha watoto wao kazi badala ya kuwapeleka shule,mabinti kuozwa mapema na watoto wa kiume kukimbilia kwenye shughuli sehemu za machimbo ya madini,yote hayo yanapaswa kufanyiwa kazi kuanzia kwa Maafisa elimu kata kwa lengo la kuboresha sekta ya elimu.


Awali akitoa utangulizi wa kikao hicho,Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali Watu,Ndg.Daniel Machunda aliyemuwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa, amesema malengo ya kikao hicho ni kupata maelekezo yake namna ya kuboresha elimu, taarifa za maendeleo ya elimu na kupokea maoni ya wadau mikakati ya kufikia malengo.

Kikao hicho kimewajumuisha wadau wa elimu 670 wakiwemo,wakuu wa Shule za Sekondari Maafisa elimu kata ,Maafisa elimu wa Halmashauri,Wakurugenzi, na baadhi ya wabunge.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti