• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AWATAKA WANANCHI WA NANSIO UKEREWE KUTUMIA MAJI SAFI NA SALAMA

Posted on: November 23rd, 2023

RC MAKALLA AWATAKA WANANCHI WA NANSIO UKEREWE KUTUMIA MAJI SAFI NA SALAMA


*Amshukuru Rais Samia kwa kutoa fedha zaidi ya Milioni 350 kuongeza Usambazaji Maji*


*Awataka MWAUWASA kutoa Elimu kwa wananchi kutunza mradi*


*Awashauri wananchi kuachana na mazoea ya kutumia Maji ya ziwani*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka wananchi wa Nansio Ukerewe kutumia maji safi na salama kutoka chanzo na kituo cha tiba ya Maji Nebuye chenye thamani ya zaidi ya Bilioni 14. 8 ili kujihakikishia afya bora na kuepukana na Magonjwa ya tumbo yatokanayo na matumizi ya Maji ya ziwani.

Mhe. Makalla amesema hayo mapema leo novemba 23, 2023 wakati wa ziara yake wilayani Nansio alipotembelea Chanzo na Kituo cha Tiba ya Maji Nebuye kilicho kwenye Usambazaji wa zaidi ya Kilomita 23.2 kwa zaidi ya Milioni 350 chini ya Mamlaka ya MajiSafi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA).


Makalla ametumia wasaa huo kumshukuru Rais Samia kwa kutoa fedha hizo ili kuboresha huduma hiyo kwa wananchi ambapo amebainisha kuwa hali ya upatikanaji wa Maji safi itaongezeka na wananchi wanapaswa kuchangamkia fursa hiyo kwa kuunganisha maji kwenye nyumba zao na kuachana na matumizi ya Maji ya ziwa.

"Maji haya ndio safi na Salama kwani yametibiwa hivyo hakuna tena magonjwa ya tumbo tukiyatumia kwa hiyo nawasihi tuachane na maji ya ziwa ambayo si salama kwa matumizi na hatarishi kwa wananchi kuliwa na mamba na viboko" Makalla.


Halikadhalika, Makalla amewataka MWAUWASA kutoa elimu kwa wananchi wa Nansio ili waumiliki mradi wao na kuweza kuutunza wakijivunia kuwa Rais Samia anauboresha kwa ajili yao hivyo wanapaswa kuutunza ili uwe na tija.

Mkurugenzi wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira (MWAUWASA) Mhandisi, Robert Lupoja amebainisha kuwa chanzo hicho cha maji kinahudumia wateja 3900 kwa sasa kwenye vituo vya maji 52 na kwamba wapo kwenye juhudi za kuondoa kabisa upotevu wa maji wa asilimia 10 uliopo kwa sasa.

"Wananchi wa Nansio tunaenda kuwaongezea huduma ya maji safi kupitia usambazaji huu mkubwa utakaotufikisha kwenye kuhudumia wananchi hadi kufikia asilimia 95 ifikapo mwaka 2024/25 hivyo tunawaomba mlipe ankara za maji kwa wakati ili tuongeze usambazaji." Amesisitiza Mkurugenzi huyo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti