• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AWATAKA WATUMISHI KUFANYA KAZI KWA BIDII ILI KULILETEA TAIFA MAENDELEO

Posted on: March 16th, 2024

RC MAKALLA AWATAKA WATUMISHI KUFANYA KAZI KWA BIDII ILI KULILETEA TAIFA MAENDELEO


*Awaasa watumishi kuwa na weledi, bidii na wazalendo kwa Taifa*


*Ataka taarifa ya utekelezaji wa shughuli kutolewa katika kila robo*


*Baraza laipongeza Idara ya Utumishi RS Mwanza kwa kujali watumishi*


Mhe. Amina Makilagi, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana amewataka Watumishi na waajiri Mkoani Mwanza kutimiza wajibu wao wa kisheria wa kuwahi kazini, kutunza mali za umma na kuwa wazalendo ili kukuza utumishi kwa pamoja na kuliletea Taifa maendeleo.

Mhe. Makilagi amesema hayo leo Machi 16, 2024 wakati akilihutubia Baraza la wafanyakazi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mkoa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza lililofanyika kwenye Ukumbi wa Wag Hill Resort chini ya Kaulimbiu ya 'Tutatue Changamoto kwa Pamoja'.

Aidha, Mhe. Makilagi amesema mpango wa bajeti katika idara ni lazima uwe shirikishi kwa watumishi ili kila mmoja ajue ni shughuli gani itatekelezwa na kwa wakati gani, na sambamba na hilo akatoa wito kwa watumishi kutofuja fedha za umma na kuepuka rushwa mahala pa kazi.

Mwenyekiti wa baraza la Wafanyakazi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza Emily Kasagara ametoa wito kwa watumishi kushirikiana katika kutimiza Dira ya maendeleo ya miaka mitano na kufanya kazi kwa bidii, weledi, juhudi na kuwa wabunifu ili kujenga Taifa uchumi wa nchi.

"Hadi kufikia mwisho wa mwaka mwezi Juni, 2023 jumla ya Sh. 478,226, 133,790 zilipokelewa sawa na asilimia 96.6 ya fedha zote zilizoidhinishwa na kwamba hiyo ni sawa na asilimia 95 ya fedha zilizopokelewa," amefafanua Mkuu wa Seksheni ya Mipango na Uratibu Henry Mwaijega.


Mwaijega ameongeza kuwa katika mwaka wa fedha 2023/24 Mkoa umeidhinishiwa kutumia zaidi ya Bilioni 487 na kwamba kumekua na ongezeko la Bilioni 16.8 sawa na asilimia 3.5 ikilinganishwa na 2022/23 huku ongezeko hilo likitokana na fedha za mishahara, matumizi mengineyo na fedha za miradi kutoka serikali kuu kuongezeka.

Halikadhalika, amewasilisha pia rasimu ya Bajeti ya Mkoa na Halmashauri zake kwa mwaka 2024/25 inayoonesha kuwa mkoa umepanga jumla ya Sh. 523, 067,403,641 kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake. zikijumuisha zaidi ya Bilioni 308 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na Bilioni 142.5 kwa shughuli za maendeleo.


Akiwasilisha taarifa za kiutawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu Bi. Franciscar Mmari amesema hadi kufikia Disemba 2023 watumishi 25 wa kada mbalimbali walipandishwa vyeo huku 5 hawakupandishwa kutokana na kukosa sifa za muundo kwa mujibu wa miundo ya maendeleo ya utumishi wa kada zao.

Aidha, ametoa rai katika uandaaji wa ikama na bajeti ya mishahara uzingatie miundo ya maendeleo ya utumishi, miundo ya mshahara, mfumo wa usimamizi wa taarifa za kiutumishi na mishahara pamoja na bajeti kutengwa na kituo cha kazi husika na si vinginevyo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti